WANAHARAKATI nchini wamepinga mpango wa Ikulu wa kutaka kuwapo na
uchunguzi wa watendaji katika wizara na taasisi nyingine za umma
wanaotuhumiwa kuhusika na ubadhirifu wa fedha za umma kwa kigezo kwamba
ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inatosha
kuwafikisha mahakamani.
Kauli hiyo imekuja baada ya juzi Ikulu
kuagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na
Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) kuwachunguza watendaji hao na kwamba
uchunguzi huo kwa kile walichoeleza ni ili kutomuonea mtu wala
kukandamiza wakati wa kuchukua hatua.
Wakichangia maoni katika
mada ya hali ya uwajibikaji nchini iliyotolewa kwenye Semina ya
Maendeleo na Jinsia (GDSS), iliyofanyika katika viwanja vya Mtandao wa
Jinsia Tanzania (TGNP) jijini Dar es Salaam walisema , tuhuma
zilizowaondoa kwenye nafasi zao ni za kushindwa kuwajibika na si za
rushwa.
Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Jinsia katika mtandao huo,
Diana Mwiru alisema
...
Read more »