PEEEEEOPLE'S POOOOOOOWEEEEEER NGUVU YA UMMAAA
Wednesday, 2024-04-17
My site
PAMOJA TUNAWEZA KULINDA TANZANIA
Site menu
Our poll
Rate my site
Total of answers: 3
Statistics

Total online: 1
Guests: 1
Users: 0
JIUNGE NA CHADEMA UOKOE RASILIMALI ZA TAIFA KAMA RASILIMALI HAZITAANZA KUWANUFAISHA WANANCHI WA ENEO HUSIKA KATIKA TAIFA KUNA HAATARI YA TAIFA KUINGIA KWENYE VURUGU KAMA ILIVYO KUWA KWA SUDANI KUSINI
Main » Entries archive






Magufuli: Sijampa Mkulo siku saba






WAZIRI wa Ujenzi, John Magufuli, amesema hajatoa siku saba kwa Waziri Mustafa Mkulo kama alivyonukuliwa na gazeti la Tanzania daima jana, akidai kutokuwa na mamlaka hayo.
Akizungumza na mwandishi wa Tanzania daima kwa njia ya simu, Magufuli alisema hawezi kutoa amri na agizo la aina hiyo kwa kuwa hana nguvu za aina hiyo kisheria, badala yake alisema amelipa siku saba Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ambalo linatakiwa kuhakikisha limeondoa nguzo ndani ya muda huo vinginevyo wataziondoa kwa nguvu.
Tanzania Daima jana liliandika pamoja na matamshi mengine, kuwa Magufuli alikuwa amempa Waziri Mkulo siku saba kuhakikisha kuwa ameruhusu kuondolewa kwa vifaa vya ujenzi bandarini vilivyozuiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) vinginevyo angemshtaki kwa Rais Kikwete.
"Nimekaa serikalini kwa muda wa miaka 1 ... Read more »

Views: 623 | Added by: twangaraha | Date: 2012-05-04 | Comments (0)

Hatma ya Opulukwa wa CHADEMA leo




MAHAKAMA ya Kuu Kanda ya Tabora imeitupa kesi ya kupinga matokeo yaliyompa ushindi mbunge wa jimbo la Kasulu Vijijini, Agripina Buyogera wa NCCR-Mageuzi.
Jaji Haruna Songoro amesema kesi hiyo imetupwa kwa kuwa upande wa walalamikaji umeshindwa kuwasilisha ushahidi wa madai yao.
Kesi hiyo ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Daniel Nsanzugwanko, akidai kuwa Buyogera alimtangaza kwamba ni mchawi na kuwa alifuja sh milioni 31 za mfuko wa jimbo.
Jaji Songoro pamoja na kutoa uamuzi huo, alimwamuru Nsanzugwanko kumlipa Buyogera gharama zote alizotumia katika kesi hiyo. Baada ya kutolewa hukumu hiyo, wafuasi wa Buyogera walimbeba juu na kuondoka naye mahakamani hapo.
Kwa upande wake Nsanzugwako ameahidi kukata rufaa kupinga hukumu hiyo, akidai kuwa jaji alionyesha upendeleo wa wazi.
Hatma ya ubunge wa Opulukwa le ... Read more »

Views: 691 | Added by: twangaraha | Date: 2012-05-04 | Comments (0)

UVCCM sasa waunda kamati kuchunguza mgogoro Arusha.


Peter Saramba, Arusha
MAKAO Makuu ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), unatarajia kutuma kamati maalumu kuchunguza na kutafuta ufumbuzi wa mgogoro unaofukuta ndani ya umoja huo mkaoni hapa.

Katibu Mkuu wa UVCCM, Martin Shigela alisema kamati hiyo itakayoongozwa na Naibu wake (Bara), Mfaume Kizigo, itawasili Arusha kati ya kesho au keshokutwa.

Akizungumza kwa simu juzi, Shigela alisema uamuzi huo unalenga kutafuta kiini cha minyukano ya mara kwa mara kati ya makundi ya vijana mkoani Arusha uliodumu kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.

"Awali, nilipanga kufika Arusha mimi binafsi kufanya ziara wilaya zote kuzungumza na viongozi na vijana wa CCM, lakini nimebadilisha mpango baada ya kuibuka kwa malumbano na matamko mbalimbali yanyotolewa na makundi yanayohasimiana ndani ya UVCCM mko ... Read more »

Views: 633 | Added by: twangaraha | Date: 2012-05-04 | Comments (0)

WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI WATUA IKULU



Wahariri waitwa Ikulu Wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo wameitwa kuwepo Ikulu Magogoni ifikapo saa 9:00 alasiri,tukio ambalo linatafsiriwa kuwa huenda ni kutangazwa



Views: 745 | Added by: twangaraha | Date: 2012-05-04 | Comments (0)

JK apandisha joto uteuzi mawaziri
Friday, 04 May 2012 09:58




Rais Jakaya KIkwete
AMTEUA MBATIA KUWA MBUNGE, MAWAZIRI WAPIGWA ‘STOP’ KUTOKA DAR
Waandishi Wetu
JOTO la mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri yanayotarajiwa kutangazwa wakati wowote kuanzia sasa limezidi kupanda kutokana na Rais Rais Jakaya Kikwete kuwateua kuwa wabunge watu watatu, akiwamo Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.

Wengine walioteuliwa ni Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Sospeter Muhongo na kada wa CCM, Janet Mbene. Taarifa iliyotolewa na Ikulu jana jioni ilisema Rais Kikwete amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya Ibara ya 66(i) (e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Taarifa hiyo ilisema uteuzi huo unaanza mara moja.

Uteuzi huo unaongeza joto la kisiasa kwani unahusishwa na mchakato unaoendelea wa mabadiliko ya Baraza la Mawaziri na jana baada ya wabunge hao kutangazwa kulikuwa na mjadala mkali katik ... Read more »
Attachments: Image 1
Views: 608 | Added by: twangaraha | Date: 2012-05-04 | Comments (0)

« 1 2 3
Login form
Calendar
«  April 2024  »
SuMoTuWeThFrSa
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
282930
NATHASON THE GREAT © 2024