PEEEEEOPLE'S POOOOOOOWEEEEEER NGUVU YA UMMAAA
Thursday, 2024-03-28
My site
PAMOJA TUNAWEZA KULINDA TANZANIA
Site menu
Our poll
Rate my site
Total of answers: 3
Statistics

Total online: 1
Guests: 1
Users: 0
JIUNGE NA CHADEMA UOKOE RASILIMALI ZA TAIFA KAMA RASILIMALI HAZITAANZA KUWANUFAISHA WANANCHI WA ENEO HUSIKA KATIKA TAIFA KUNA HAATARI YA TAIFA KUINGIA KWENYE VURUGU KAMA ILIVYO KUWA KWA SUDANI KUSINI
Main » 2012 » May » 4 » Hatma ya Opulukwa wa CHADEMA leo
4:51 PM
Hatma ya Opulukwa wa CHADEMA leo

Hatma ya Opulukwa wa CHADEMA leo




MAHAKAMA ya Kuu Kanda ya Tabora imeitupa kesi ya kupinga matokeo yaliyompa ushindi mbunge wa jimbo la Kasulu Vijijini, Agripina Buyogera wa NCCR-Mageuzi.
Jaji Haruna Songoro amesema kesi hiyo imetupwa kwa kuwa upande wa walalamikaji umeshindwa kuwasilisha ushahidi wa madai yao.
Kesi hiyo ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Daniel Nsanzugwanko, akidai kuwa Buyogera alimtangaza kwamba ni mchawi na kuwa alifuja sh milioni 31 za mfuko wa jimbo.
Jaji Songoro pamoja na kutoa uamuzi huo, alimwamuru Nsanzugwanko kumlipa Buyogera gharama zote alizotumia katika kesi hiyo. Baada ya kutolewa hukumu hiyo, wafuasi wa Buyogera walimbeba juu na kuondoka naye mahakamani hapo.
Kwa upande wake Nsanzugwako ameahidi kukata rufaa kupinga hukumu hiyo, akidai kuwa jaji alionyesha upendeleo wa wazi.
Hatma ya ubunge wa Opulukwa leo
Wakati huohuo Mahamaka Kuu Kanda ya Tabora, leo itatoa hukumu ya kesi ya kupinga matokeo ya ubunge wa jimbo la Meatu mkoani Simiyu, yaliyompa ushindi, Meshack Opulukwa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Kesi hiyo namba 1/2010 ilifunguliwa na mpiga kura, Masanja Renatus Salu, ambaye analalamikia ushindi wa Opulukwa kutokana na kuwepo kwa dosari katika uchaguzi huo.
Katika hati ya malalamiko, Salu anamlalamikia Opulukwa kutumia lugha ya ubaguzi dhidi ya mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Salum Khamis.
Madai mengine ni kuwa baadhi ya wasimamizi wasaidizi katika vituo nane walimpigia kampeni mbunge huyo na msimamizi wa uchaguzi kutangaza matokeo mara mbili kinyume cha taratibu za Tume ya Uchaguzi.
Katika kesi hiyo iliyokuwa ikisikilizwa na Jaji Frederick Wambali, upande wa mlalamikaji ulileta mahakamani hapo mashahidi 15 ili kuthibitisha madai yao huku upande wa utetezi ukileta mashahidi tisa.
Katika mwenendo wa kesi hiyo, wananchi wengi waliokuwa wakiisikiliza kutoka katika maeneo mbalimbali ya wilaya za Meatu, Bariadi, Maswa na Shinyanga, wanataka kujua hatma yake leo.
Walalamikiwa katika kesi hiyo ni watatu ambao ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Opulukwa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Meatu.
Mlalamikaji alikuwa akiwakilishwa wa wakili wa kujitegemea, Kamaliza Kayaga, wakati Opulukwa alikuwa akiwakilishwa na wakili pia wa kujitegemea, Godwin Mganyizi.



Views: 688 | Added by: twangaraha | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
Name *:
Email *:
Code *:
Login form
Calendar
«  May 2012  »
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031
NATHASON THE GREAT © 2024