PAMOJA TUNAWEZA KULINDA TANZANIA
Statistics |
Total online: 1 Guests: 1 Users: 0 |
JIUNGE NA CHADEMA UOKOE RASILIMALI ZA TAIFA
KAMA RASILIMALI HAZITAANZA KUWANUFAISHA WANANCHI WA ENEO HUSIKA KATIKA TAIFA KUNA HAATARI YA TAIFA KUINGIA KWENYE VURUGU KAMA ILIVYO KUWA KWA SUDANI KUSINI
|
Main » 2012 » May » 11 » huyu hapa white hair (lowassa)
10:39 AM huyu hapa white hair (lowassa) |
Lowassa awatuliza wanaCCM wasihamie Chadema |
|
| MBUNGE
wa Monduli, Edward Lowassa, amekuwa na mikutano ya ndani katika jimbo
lake katika kile kinachoonekana kuwa ni jitihada za kutuliza wimbi la
wana CCM kuhamia Chadema.
Katika siku za hivi karibuni kumekuwa
na wimbi la wanaCCM katika mikoa mbalimbali kuhamia Chadema. Mkoa wa
Arusha ndiyo unaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wanachama wa CCM
wanaojiunga na Chadema. Jana Lowassa ambaye aliwahi kuwa Waziri Mkuu
kabla ya kujiuzulu, alifanya mkutano wa ndani katika eneo la Mto wa Mbu
na baadaye kufuatiwa na mkutano wa hadhara.
Katika mkutano huo
wa hadhara, mbunge huyo aliwaambia wananachi kuwa pamoja na kuwa suala
la kujiunga na chama chochote cha siasa ni haki ya mtu, lakini haoni
umuhimu wa wana CCM kwa sasa kuhama chama hicho kinachotawala.
Alisema
CCM ni chama chenye kutetea maslahi ya wanyonge na kwamba kuna haja
kwa wananchi kutathimini ili kuona kama kweli CCM imeshindwa kutimiza
malengo yake.
Alisema CCM imekuwa ikitekeleza kwa vitendo
mchango wa Baba wa Taifa Mwalimu Jiulius Nyerere ambao nni umoja na
mshikamano, vinavyoifanya Tanzania kuendelea kuwa kisiwa cha amani. Lowassa pia alisema CCM ni chama kinachotetea maslahi na rasilimali za nchi ili zisiporwe na wageni.
Amewakumbusha
kuwa CCM ni chama kinachotoa nafasi kwa wanachama wake kuwa na haki ya
kuchagua na kuchaguliwa bila ya mizengwe au ubaguzi wa rangi, ukabila au
dini.
|
|
Views: 2074 |
Added by: twangaraha
| Rating: 0.0/0 |
|
|
|