PAMOJA TUNAWEZA KULINDA TANZANIA
Statistics |
Total online: 1 Guests: 1 Users: 0 |
JIUNGE NA CHADEMA UOKOE RASILIMALI ZA TAIFA
KAMA RASILIMALI HAZITAANZA KUWANUFAISHA WANANCHI WA ENEO HUSIKA KATIKA TAIFA KUNA HAATARI YA TAIFA KUINGIA KWENYE VURUGU KAMA ILIVYO KUWA KWA SUDANI KUSINI
|
Main » 2012 » May » 11 » Ikulu yaagiza uchunguzi watendaji wizarani, taasisi
10:31 AM Ikulu yaagiza uchunguzi watendaji wizarani, taasisi |
IKULU imeiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na
Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), kuwachunguza
watendaji katika wizara na taasisi nyingine za umma ambao ndio chanzo
cha mawaziri wao kuwajibishwa.
Hii ni kauli ya kwanza ya Ikulu,
tangu Rais Jakaya Kikwete afanye mabadiliko katika Baraza lake la
Mawaziri kwa kuwaondoa mawaziri sita ambao wizara zao zilitajwa kwenye
Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)
kukabiliwa na kashfa ya ufisadi na matumizi mabaya yafedha za umma.
Katibu
Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue juzi aliliambia Mwananchi kuwa
tuhuma zote ambazo zilibainishwa katika ripoti ya CAG katika maeneo
mbalimbali sasa zitachunguzwa na Takukuru pamoja na DCI. "Tuhuma zote
zitapitiwa na vyombo husika (Takukuru na DCI), kitakachofanyika ni
kuzipitia tuhuma zote ili kuwatambua wahusika sahihi,” alisema Balozi
Sefue. Alifafanua kwamba uchunguzi huo unafanyika ili kuhakikisha kuwa
uamuzi utakaotolewa haumuonei mtendaji yoyote. "Tutachunguza na
watakaobainika watakachukuliwa hatua za kinidhamu au kufikishwa
mahakamani,”alisema Sefue na kuongeza:
"Baada ya Takukuru na DCI
kumaliza kazi yao taarifa watakazozitoa zitakwenda kwa DPP (Mkurugenzi
wa Mashtaka), ili kuona kama jambo lililobainika linaweza kuchukuliwa
hatua za kinidhamu au kupelekwa mahakamani.” Balozi Sefue alisisitiza
kwamba inafanyika hivyo ili, kuhakikisha hakuna mtendaji yoyote
atakayeonewa na pia hawataki mwenye makosa aponyoke. Aliwataka
watumishi na watendaji katika wizara na taasisi nyingine za umma kufanya
kazi kwa kukumbuka mambo mawili, ambayo ni kutambua kuwa wameajiriwa
kwa ajili ya Watanzania na kuzingatia maadili ya kazi.
"Wakitekeleza
hayo mawili mambo yanakuwa mazuri zaidi…, mtumishi anatakiwa kutambua
kuwa kaajiriwa na wananchi hivyo anatakiwa kujituma na kuzingatia
maadili ya kazi,” alisisitiza Balozi Sefue. Hata hivyo, imewatoa hofu
watendaji wote nchini kwa kuwataka kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia
maadili ikiwa ni pamoja na kukumbuka kuwa wapo kazini kwa ajili ya
kuwatumikia Watanzania na si vinginevyo.
Asifia uwazi Balozi
Sefue alisema sio kweli kuwa hivi sasa vitendo vya ubadhirifu wa mali
za umma vimeongezeka bali hali hiyo inaonekana zaidi kwa sasa kwa kuwa
Serikali imekuwa ikifanya mambo yake kwa uwazi mkubwa. "Hivi sasa
ripoti mbalimbali zinawekwa wazi bungeni na wabunge wanachangia, ripoti
haziwekwi tena kabatini na hiyo ndio sababu, sio kweli kuwa matukio ya
ubadhirifu yameongezeka kwa sasa,” alifafanua Balozi Sefue. Kauli ya
balozi Sefue inakuja wakati tayari CAG , Ludovick Utouh amewaonya
mawaziri wapya na watendaji serikalini kwamba ripoti zake hivi sasa zina
nguvu za kusimamia uwajibikaji hivyo, wanapaswa kusimamia vema wizara
zao kuzuia ubadhirifu wa fedha za umma.
Utouh alisema mawaziri
wanapaswa kufahamu kuanzia sasa hadi mwaka 2015 zitatoka ripoti nyingine
tatu, hivyo ni vyema wakachukua tahadhari kama wasimamizi wakuu wa
shughuli za wizara.
Utouh alisema kilichotokea bungeni na hadi
kufikia mawaziri kuwajibishwa, imethibitisha kuwa sasa kutakuwa na
uwajibikaji mkubwa utakaosababishwa na ripoti zake kama watendaji
wasipofuata taratibu za Serikali. Wakati akitangaza mabadiliko ya
mawziri, Rais Kikwete alisema baada ya mawaziri kuwajibika kisiasa,
wanaofuta ni watendaji katika wizara na taasisi nyingine za umma ambao
ndiyo chanzo cha mawaziri hao kujiuzulu.
Alisema mawaziri
wamekuwa wakijiuzulu hata kwa makosa ambayo si yao na kwamba hivi sasa
Serikali itaanza kuchukua hatua kwa watendaji wakiwamo makatibu wakuu,
wakurugenzi wa wizara, watendaji wakuu wa mashirika na taasisi za umma
pamoja na bodi za mashirika husika.
Mawaziri waliowajibishwa
kutokana na matokeo ya ripoti ya CAG ni William Ngeleja (Nishati na
Madini), Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii), Omar Nundu (Uchukuzi),
Mustafa Mkulo (Fedha), Dk Hadji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii) na Dk
Cyril Chami (Viwanda na Biashara). Naibu Mawaziri waliokubwa pia na
panga hilo ni Dk Lucy Nkya, (Afya) na Athuman Mfutakamba (Uchukuzi).
|
Views: 635 |
Added by: twangaraha
| Rating: 0.0/0 |
|
|
|