<?xml version="1.0" encoding="UTF-8" ?>
<rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom">
	<channel>
		<title>joseph</title>
		<link>http://siasa.ucoz.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Mon, 21 May 2012 21:38:12 GMT</lastBuildDate>
		<generator>uCoz Web-Service</generator>
		<atom:link href="https://siasa.ucoz.com/news/rss" rel="self" type="application/rss+xml" />
		
		<item>
			<title>Pigo CCM uchaguzi 2015</title>
			<description>CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemaliza uchaguzi katika ngazi ya mashina na
 matawi huku kikikabiliwa na tatizo la kupata wagombea nafasi ya 
mabalozi wa nyumba kumi katika maeneo mbalimbali nchini.Uchunguzi wa 
gazeti hili katika mikoa mbalimbali, umebaini kuwa makada wengi wa CCM 
walikwepa kugombea nafasi hiyo jambo lililofanya walazimishane na kuleta
 wakati mgumu kupata warithi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kwa mujibu wa Katiba ya CCM, 
mabalozi au wajumbe wa shina ndio ngazi ya kwanza ya uongozi ndani ya 
chama hicho pia ni kiungo muhimu kati ya chama na wananchi katika maeneo
 wanayoishi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mbali ya majukumu mengine, mabalozi wa nyumba kumi 
wamekuwa wahamasishaji wakuu wa chama katika maeneo yao, kuhakikisha 
wanachama wanajiandikisha kwenda kupiga kura pia kujua idadi yao kwenye 
eneo husika.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Katibu wa CCM Wilaya ya Dodoma Mjini, Augustino 
Mbogo, amekiri kuwa kazi ya kuchagua mabalozi wa nyumba kumi iliingia 
dosari na kufanya baadhi ya watu kususa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Hata hivyo, aliwarushia 
lawama ...</description>
			<content:encoded>CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemaliza uchaguzi katika ngazi ya mashina na
 matawi huku kikikabiliwa na tatizo la kupata wagombea nafasi ya 
mabalozi wa nyumba kumi katika maeneo mbalimbali nchini.Uchunguzi wa 
gazeti hili katika mikoa mbalimbali, umebaini kuwa makada wengi wa CCM 
walikwepa kugombea nafasi hiyo jambo lililofanya walazimishane na kuleta
 wakati mgumu kupata warithi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kwa mujibu wa Katiba ya CCM, 
mabalozi au wajumbe wa shina ndio ngazi ya kwanza ya uongozi ndani ya 
chama hicho pia ni kiungo muhimu kati ya chama na wananchi katika maeneo
 wanayoishi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mbali ya majukumu mengine, mabalozi wa nyumba kumi 
wamekuwa wahamasishaji wakuu wa chama katika maeneo yao, kuhakikisha 
wanachama wanajiandikisha kwenda kupiga kura pia kujua idadi yao kwenye 
eneo husika.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Katibu wa CCM Wilaya ya Dodoma Mjini, Augustino 
Mbogo, amekiri kuwa kazi ya kuchagua mabalozi wa nyumba kumi iliingia 
dosari na kufanya baadhi ya watu kususa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Hata hivyo, aliwarushia 
lawama baadhi ya watendaji ndani ya chama hicho kwa ngazi ya Kata na 
Matawi kuwa walikuwa&amp;nbsp; kikwazo cha kukwamisha mchakato huo na kuwafanya 
baadhi ya wanachama&amp;nbsp; kususa.&lt;br&gt;Mbogo alitoa kauli hiyo jana alipokuwa 
akielezea namna mchakato wa uchaguzi ndani ya chama unavyoendelea, 
ikiwemo uchaguzi wa ngazi ya mashina ambao umefikia kilele hivi 
karibuni.&lt;br&gt;Alisema kuwa katika wilaya yake, yako maeneo ambayo 
viongozi walitoa taarifa kuwa mabalozi walikuwa wakikataa kugombea na 
maeneo mengine waliamua kupeana nafasi hizo bila kufuata taratibu 
zozote.&lt;br&gt;&quot;Ni kweli kuna baadhi ya maeneo hali haikuwa nzuri, mfano 
Kata za Chihanga,Hombolo na Mtumba tumepata wakati mgumu watu waligoma 
kugombea nafasi hizo,’’alisema Mbogo.&lt;br&gt;Kiongozi huyo alibainisha 
sababu za wanachama kugomea kugombea nafasi hizo ambapo alisema ni 
kutokana na ukiritimba mkubwa uliokuwa ukifanywa na baadhi ya makatibu 
wa maeneo husika.&lt;br&gt;&quot;Unajua wale viongozi wa ngazi ya chini ni watu wa 
kuchaguliwa, hivyo katika maeneo mengi walikuwa wakipanga safu zao ili 
kujijenga na kuwa na mtaji wa wapiga kura pindi watakapoanza kugombea na
 wao,’’alisema.&lt;br&gt;Alitolea mfano kuwa baadhi ya maeneo fomu za kugombea
 nafasi hizo za mashina zilikuwa zikiuzwa kati ya Sh 5000 hadi 10,000 
kinyume na utaratibu jambo lililofanya baadhi ya watu kushindwa 
kuzinunua.&lt;br&gt;Wakati Katibu huyo akieleza mchakato huo, uchunguzi 
uliofanywa katika baadhi ya maeneo umebainisha kuwa kwa baadhi ya 
sehemu, nafasi hizo hazikutangazwa kabisa,hivyo kufanya mabalozi 
waliokuwa madarakani waendelee kuongoza hata kama muda umepita.&lt;br&gt;Kata 
za Nzuguni, Iyumbu, Makutupora pamoja na maeneo ya Mpunguzi, Zuzu na 
maeneo kadhaa ya mjini Dodoma, uchaguzi huo haukufanyika na wengi 
hawajui kama mwaka huu ulikuwa ni mwaka wa uchaguzi kwa mabalozi.&lt;br&gt;Kamati ya siasa Arusha yakutana &lt;br&gt;&lt;br&gt;Uchaguzi
 wa Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) wa mashina, matawi na mabalozi 
katika wilaya tano za mkoa wa Arusha, umeelezwa kudorora&amp;nbsp; kwa kiasi 
kikubwa mwaka huu, huku wilaya za Arusha mjini na Arumeru zikishindwa&amp;nbsp; 
kabisa kufanya uchaguzi wa matawi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Habari za uhakika kutoka ndani
 ya chama hicho, ambazo zimethibitishwa na Katibu wa Uenezi na Itikadi 
wa CCM Mkoa wa Arusha, Loota Sanare, zimebainisha kuwa, kudorora kwa 
chaguzi hizo kumesababisha na sababu mbali mbali ikiwepo hali ya kisiasa
 mkoani Arusha.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Sababu nyingine zilizotajwa&amp;nbsp; na&amp;nbsp; baadhi ya 
viongozi wa CCM wa wilaya&amp;nbsp; mkoani hapa, ni pamoja na&amp;nbsp;&amp;nbsp; kukosekana 
wagombea, na hivyo viongozi waliopo kuendelea kushikilia nafasi zao na 
kushindwa kusimamiwa zoezi la uchukuaji fomu, kurejeshwa na kupitisha 
majina kutokana na viongozi wengi kushiriki katika uchaguzi mdogo wa 
jimbo la Arumeru.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kwa mujibu wa taarifa hizo, uchaguzi wa matawi 
katika wilaya hasa za Arusha na Arumeru hadi jana ulikuwa haujafanyika, 
wakati uchaguzi wa mashina na mabalozi pia haujafanyika kwani wengi wa 
mabalozi, wameendelea na nafasi zao.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Unajua mwaka huu, hapa 
Arusha tulikuwa na uchaguzi wa Arumeru kuanzia Januari hadi Aprili 
viongozi wengi walikuwa huko, hivyo ilishindikana uratibu wa 
chaguzi,&quot;alisema kiongozi huyo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Hata hivyo, alisema katika wilaya
 nyingine za Longido, Monduli, Karatu na Ngorongoro, uchaguzi wa ngazi 
za Mashina na matawi zimefanyika kwa wastani wa asilimia 80 tu.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kutokana
 na hali hiyo, Kamati ya Siasa Mkoa wa Arusha, ilitarajiwa kukutana jana
 kupokea taarifa za chaguzi hizo na kujua uhai wa chama katika wilaya 
zote.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Sanare alisema katika kikao hicho, kila wilaya itakuwa na 
ripoti yake ya chaguzi, hivyo kujulikana taarifa sahihi ni maeneo gani 
hazijafanyika na sababu zake, pia hatua ambazo zitachukuliwa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Naomba
 usubiri mara baada ya kikao cha Kamati ya Siasa tutakuwa na taarifa 
kamili ya chaguzi hizo na hali ya kisiasa ya mkoa wetu,&quot;alisema Sanare.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mkoa
 wa Arusha ni miongoni mwa mikoa ambayo hali ya kisiasa imekuwa tete kwa
 CCM hasa kutokana na viongozi wake na makada kadhaa kujiengua na 
kujiunga na chadema.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kinondoni&lt;br&gt;&lt;br&gt;Akizungumza jana Mwenyekiti
 wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Aron Mwaikambo alisema chaguzi zilizo 
tayari ni za jumuiya pamoja na chama ngazi ya ubalozi na matawi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mwaikambo
 alisema, ubalozi wa nyumba kumi tangu Februari mwaka huu ila hapakuwa 
na upinzani kwa sababu sehemu nyingi ni mtu mmoja tu alijitokeza 
kugombea, hivyo kushinda bila upinzani.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&amp;nbsp;&quot;Tulifanya uchaguzi wa 
nyumba kumi kuanzia Februari 2 hadi 5 mwaka huu tukamaliza zoezi hilo na
 tulipenda&amp;nbsp; kungekuwepo na upinzani ila watu walikua wachache na katika 
kila eneo la hizo nyumba kumi aliyechukua fomu ndio mshindi kwasababu&amp;nbsp; 
hapakua na upinzani kabisa”alisema Mwaikambo.Alieleza:&lt;br&gt;&lt;br&gt;Sehemu 
nyingi wazee wamechoka hivyo wamewaachia vijana nafasi hiyo lakini 
asilimia kubwa ya vijana hawakujitokeza kwani licha ya balozi kuwa 
anatekeleza kazi za chama, pia ana jukuma la kupatanisha migogoro 
inayotokea katika nyumba hizo hasa familia ambapo kwa vijana inakua 
ngumu.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Temeke&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wakati hayo yakiendelea Kinondoni Msemaji wa
 CCM Wilaya ya Temeke, Saad Kusilawe amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi 
kimepata watu wengi waliojitokeza kuchukua fomu za ubalozi wa nyumba 
kumi katika kata zake zote.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Akizungumza jana ofisini kwake, 
alisema hali ilikuwa tofauti na alivyofikiria kwani waliojitokeza ni 
wengi tofauti na kipindi cha nyuma kulikuwa na wanachama wapatao 5,228 
na katika kipindi hiki waliokuja kuchukuwa fomu hizo wamefikia 7,800 
hali ambayo inaonyesha kuwa chama hicho bado kipo imara.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kusilawe
 alisema hali ya siasa ina changamoto hasa kipindi hiki ambacho vijana 
wengi wamejikita katika suala la siasa&amp;nbsp; na kupelekea mambo kubadilika 
kutokana na kujitambua kwao.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;kwakweli vijana wamekuja juu sana 
kipindi hiki ila kinachoniogopesha ni kuhusu kuja kwao juu ni kwa 
kuchochewa na baadhi ya wanasiasa kufanya fujo na siyo kujenga nchi kama
 inavyofikiriwa”alisema kusilawe.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Aliongeza kuwa vijana wengi 
hivi sasa wamekaa kiushawishi na mara nyingi uacha mambo yanayowapeleka 
shule na kuanza kufanya siasa ambayo mara nyingi inakuwa ni hasara kwao 
kutokana na fujo wanazo zianzisha. &lt;br&gt;&amp;nbsp;&lt;br&gt;Dodoma&lt;br&gt;Katibu wa Chama 
Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma Mjini, Augustino Mbogo amekiri kuwa
 kazi ya kuchagua mabalozi wa nyumba kumi iliingia dosari na kufanya 
baadhi ya watu kususa.&lt;br&gt;Hata hivyo,&amp;nbsp; aliwarushia lawama baadhi ya 
watendaji ndani ya chama hicho kwa ngazi ya Kata na Matawi kuwa walikuwa
 ni kikwazo cha kukwamisha mchakato huo na kuwafanya baadhi ya watu 
kususia.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mbogo alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akielezea namna 
mchakato wa uchaguzi ndani ya chama unavyoendelea ikiwemo uchaguzi wa 
ngazi ya mashina ambao umefikia kilele mwishoni mwa wiki.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alisema
 kuwa katika wilaya yake yako maeneo ambayo viongozi walitoa taarifa 
kuwa mabalozi walikuwa wakikataa kugombea na maeneo mengine waliamua 
kupeana nafasi hizo bila kufuata taratibu zozote.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Ni kweli kuna 
baadhi ya maeneo hali haikuwa nzuri, mfano Kata za Chihanga, Hombolo na 
Mtumba tumepata wakati mgumu watu waligoma kugombea nafasi 
hizo,’’alisema Mbogo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kiongozi huyo alibainisha sababu za 
wanachama kugomea kugombea nafasi hizo ambapo, alisema ni kutokana na 
ukiritimba mkubwa uliokuwa ukifanywa na baadhi ya makatibu wa maeneo 
husika.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Unajua wale viongozi wa ngazi ya chini ni watu wa 
kuchaguliwa, hivyo katika maeneo mengi walikuwa wakipanga safu zao ili 
kujijenga na kuwa na mtaji wa wapiga kura pindi watakapoanza kugombea na
 wao,’’alisema.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alitolea mfano kuwa baadhi ya maeneo fomu za 
kugombea nafasi hizo za mashina zilikuwa zikiuzwa kati ya Sh 5000 hadi 
10,000 kinyume na utaratibu jambo lililofanya baadhi ya watu kushindwa 
kuzinunua.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wakati Katibu huyo akieleza mchakato huo, uchunguzi 
uliofanywa katika baadhi ya maeneo umebainisha kuwa katika maeneo mengi 
nafasi hizo hazikutangazwa kabisa, hivyo kufanya mabalozi waliokuwa 
madarakani waendelee kuongoza hata kama muda umepita.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Hofu ya 
kutotangaza inatokana na ukweli kuwa baadhi ya mabalozi hawapendi 
kuendelea kuongoza na hivyo kama nafasi hizo zingetangazwa, ni wazi kuwa
 wangeweza kuziachia huku chama kikikosa mgombea katika eneo husika.&lt;br&gt;Kata
 za Nzuguni, Iyumbu, Makutupora pamoja na maeneo ya Mpunguzi,Zuzu na 
maeneo kadhaa ya mjini Dodoma, uchaguzi huo haukufanyika na wengi 
hawajui kama mwaka huu ulikuwa ni mwaka wa uchaguzi kwa mabalozi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mara&lt;br&gt;Uchaguzi
 ngazi ya mashina na matawi ya&amp;nbsp; ya CCM umeshindwa kufanyika katika 
maeneo mbalimbali wilayani Serengeti ,kutokana na wanachama wengi kususa
 kujitokeza, hali iliyosababisha watu wateuliwe kushika ubalozi kinyume 
na utaratibu wa kawaida wa chama wa kupigiwa kura.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Uchunguzi wa 
Mwananchi Jumapili ulibaini kuwa nafasi nyingi za ubalozi wa mashina&amp;nbsp; 
zimekimbiwa na wanachama wa CCM na sasa waliotayari wanateuliwa kujaza 
nafasi hizo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Hii ni aibu kubwa na haijawahi kutokea maana ilipofika kipindi hiki cha uchaguzi, watu walifukuzana kuwania ubalozi&lt;br&gt;,lakini
 leo mtu akionekana anachukua fomu ya ubalozi watu wanamzoea, hakika 
chama kinakwenda pabaya,”alisema Katibu mmoja wa Tawi la CCM, jina 
limehifadhiwa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Katika Kata ya Manchira, mbali na uteuzi wa 
mabalozi na wengine kukataa uteuzi hata uchaguzi wa viongozi ngazi ya 
tawi uliokuwa ufanyike mwishoni mwa wiki hii ulishindikana baada ya 
wanachama wakiwemo waliochukua fomu, kutojitokeza.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Habari za 
uhakika na zilizothibitishwa na baadhi ya viongozi wa matawi na Kata wa 
chama hicho, zinadai katika Tawi la Rwamchanga, walijitokeza watu 
wasiozidi wanane, hali iliyomlazimisha Katibu wa Uchumi wa Kata hiyo, 
John Wambura ambaye alikuwa msimamizi, kuahirisha hadi Mei 21 mwaka huu.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Hali hiyo pia iliyakumba matawi ya Ntamyo,Miserere na Miseke&lt;br&gt;ambapo
 wanachama hawakujitokeza hata waliojaza fomu za kuwania nafasi 
mbalimbali ,huku kukiwa na uvumi kuwa wana mpango wa kujiungua Chadema 
na wanasubiri viongozi wa kitaifa wahame.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mwenyekiti wa CCM 
Wilaya, Patrick Chandi alikiri kuwepo kwa migogoro baadhi ya maeneo 
ambapo amelazimika kumwagiza Katibu wake wa wilaya kufuatilia chanzo cha
 matatizo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Kwa ujumla tunaendelea ingawa kuna mambo hayawezi kwenda sawa sawa.&lt;br&gt;Maeneo kama Rwamchanga,Tamukeri ,Kisaka na kwingineko kuna migogoro ya ndani kwa ndani,”alisema.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&lt;br&gt;</content:encoded>
			<link>https://siasa.ucoz.com/news/pigo_ccm_uchaguzi_2015/2012-05-22-30</link>
			<dc:creator>twangaraha</dc:creator>
			<guid>https://siasa.ucoz.com/news/pigo_ccm_uchaguzi_2015/2012-05-22-30</guid>
			<pubDate>Mon, 21 May 2012 21:38:12 GMT</pubDate>
		</item>
		<item>
			<title>shibuda, mwana ccm aliye tumwa kuichafua chadema</title>
			<description>SAKATA la Mbunge wa Maswa Mashariki, John Shibuda kutangaza nia ya 
kuwania urais ndani ya Kikao cha Halmashauri Kuu (Nec) ya CCM, sasa 
linaitikisa Chadema baada ya Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la 
chama hicho (Bavicha), Joliana Shonza kupingana hadharani na bosi wake, 
John Heche. &lt;p&gt;Wakati Heche akiwa tayari ametoa tamko kumshambulia 
Shibuda akisema chama hicho hakitaruhusu mgombea wake urais&amp;nbsp; atangaze 
nia kwenye vikao vya CCM, Shonza ameibuka na kusema tamko hilo la bosi 
wake siyo la Bavicha ila ni lake binafsi.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Jana, Shonza akizungumza
 na waandishi wa habari Dar es Salaam, alilikana tamko la Heche wiki 
iliyoipita akisema hakuna kikao ambacho baraza hilo lilikaa na kutoa 
kauli moja kumjadili Shibuda.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Hii ni mara ya tatu kwa Shibuda 
kusababisha mgongano ndani ya Chadema. Aliwahi kupinga msimamo wa 
kutotambua matokeo ya urais wa Jakaya Kikwete na badala yake, alishiriki
 tafrija Ikulu ndogo Chamwino, baada ya mkuu huyo wa nchi kuzindua Bunge
 la 10 n...</description>
			<content:encoded>SAKATA la Mbunge wa Maswa Mashariki, John Shibuda kutangaza nia ya 
kuwania urais ndani ya Kikao cha Halmashauri Kuu (Nec) ya CCM, sasa 
linaitikisa Chadema baada ya Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la 
chama hicho (Bavicha), Joliana Shonza kupingana hadharani na bosi wake, 
John Heche. &lt;p&gt;Wakati Heche akiwa tayari ametoa tamko kumshambulia 
Shibuda akisema chama hicho hakitaruhusu mgombea wake urais&amp;nbsp; atangaze 
nia kwenye vikao vya CCM, Shonza ameibuka na kusema tamko hilo la bosi 
wake siyo la Bavicha ila ni lake binafsi.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Jana, Shonza akizungumza
 na waandishi wa habari Dar es Salaam, alilikana tamko la Heche wiki 
iliyoipita akisema hakuna kikao ambacho baraza hilo lilikaa na kutoa 
kauli moja kumjadili Shibuda.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Hii ni mara ya tatu kwa Shibuda 
kusababisha mgongano ndani ya Chadema. Aliwahi kupinga msimamo wa 
kutotambua matokeo ya urais wa Jakaya Kikwete na badala yake, alishiriki
 tafrija Ikulu ndogo Chamwino, baada ya mkuu huyo wa nchi kuzindua Bunge
 la 10 na pia, aliwahi kupinga msimamo wa chama hicho kukataa posho 
bungeni badala yake alitaka ziongezwe hadi Sh500,000 huku akiziita ni, 
&quot;ujira wa mwiha” na kuwarushia makombora baadhi ya viongozi wake akisema
 ni wabunge wafanyabiashara.&amp;nbsp; &amp;nbsp;&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Katika sakata hilo la sasa, Shonzi
 alisema: &quot;Naomba ifahamike kwamba tamko alilolitoa Heche siyo la 
Baraza, bali ni lake kama Heche. Alipokuwa akitoa tamko hilo hakukuwa na
 kikao chochote cha Baraza cha viongozi wa kitaifa wala Sekretarieti ya 
Baraza la Vijana la Chadema ili kulijadili suala hili kwa kina bali, 
alitumia mwamvuli wa vijana kuhalalisha hoja yake.”&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Shonza alisema
 tamko alilolitoa dhidi ya Shibuda liliandaliwa na kuandikwa na Ofisa 
Habari wa Chadema Makao Makuu,&amp;nbsp; kitu ambacho ni kinyume na utaratibu na 
kanuni za Bavicha.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;&quot;Bavicha tumejikamilisha kwa maana ya kwamba, 
tuna uongozi wetu kamili wa taifa. Tuna ofisi zetu ambazo ni nje ya 
ofisi za makao makuu sasa iweje tamko hilo likaandaliwe makao makuu tena
 na mtu ambaye hahusiki na Bavicha?”&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Shonza alisema kama utaratibu
 huo alioutumia Heche ungekuwa unatumiwa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk 
Willibrod Slaa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe kufanya uamuzi binafsi&amp;nbsp;
 pasipo kuyajadili na sekretarieti ya chama, wasingeweza kufikia matunda
 yanayoonekana hivi sasa.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;&lt;strong&gt;Msimamo wa Heche&lt;/strong&gt;&lt;br&gt;Wakati
 Makamu huyo akimrushia makombora bosi wake, jana Heche naye alitoa 
tamko akisema: &quot;Natoa taarifa kwa umma kwamba baada ya mashauriano, 
Katibu wa Bavicha, Deogratias Siale ameitisha kikao cha sekretariati 
taifa Alhamisi, Mei 24, 2012, kwa ajili ya kujadili na kuwasilisha 
mapendekezo kwenye vikao halali vya chama kwa ajili ya hatua zaidi.”&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Aliongeza,
 &quot;Wakati huohuo, nimejulishwa kuwa Makamu wangu (Shonza), leo 
amezungumza na vyombo vya habari na kukanusha taarifa niliyotoa kwa 
niaba ya Bavicha. Itambulike kuwa majukumu na mamlaka ya mwenyekiti na 
kiongozi mwingine yeyote wa Baraza&amp;nbsp;yanabainishwa na Kanuni za Baraza 
letu&amp;nbsp;kifungu 5.4.1, ambayo mwenyekiti ndiye msemaji mkuu wa Baraza na 
pia ndiye kiongozi mkuu wa Baraza katika ngazi husika.”&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Alisema 
kifungu cha 5.4.2 kinabainisha majukumu ya makamu mwenyekiti ambaye 
anapaswa kufanya kazi chini ya mwenyekiti na ndiye msaidizi wake.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Alisema
 Katiba ya chama ambayo ndiyo msingi mama wa shughuli za Baraza katika 
kanuni zake kifungu cha 7.7.1, inabainisha kazi za mwenyekiti na pia 
anaweza kufanya nini na wakati gani kwa kushauriana na nani.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;&quot;Kwa 
kutumia kifungu hiki, nilipokea ushauri kutoka kwa viongozi mbalimbali 
wa Bavicha, akiwemo makamu mwenyekiti na kushauriana na Katibu na kuona 
haja ya kutoa kauli na mwongozo wa nini kitafuata kwa niaba ya baraza 
kama hatua ya kwanza,” alisema na kuongeza:&lt;/p&gt;&lt;p&gt;&lt;strong&gt;Bavicha Shinyanga&lt;/strong&gt;&lt;br&gt;Bavicha
 Mkoa wa Shinyanga nalo jana limetoa tamko na kumkosoa Shibuda. Tamko 
hilo lililotolewa na Mwenyekiti wake, Nzemo Renatus, lilisema: &quot;Tatizo 
letu na Shibuda ni kutoa kauli hii huku katiba ya Chadema na taratibu 
zake anazifahamu. &lt;/p&gt;&lt;p&gt;Lakini mbaya zaidi anakidhalilisha chama kwa 
kutoa kauli nzito katika kikao cha mahasimu wetu wakuu wa kisiasa,&amp;nbsp; CCM 
huku akiwa mwanachama wetu. Ni sawa na mvuvi anayetoboa mtumbwi wake 
mwenyewe akiwa katikati ya Ziwa au Bahari.”&lt;/p&gt;&lt;p&gt;&amp;nbsp;&quot;Kwa niaba ya Bavicha
 Mkoa wa Shinyanga, naungana na kauli ya Mwenyekiti wa Bavicha Taifa. 
Tunaomba aitishe kamati ya utendaji ya Taifa haraka iwezekanavyo tuweze 
kupitisha maazimio ya kauli tatanishi za Mbunge Shibuda.”&lt;/p&gt;

&lt;br&gt;</content:encoded>
			<link>https://siasa.ucoz.com/news/shibuda_mwana_ccm_aliye_tumwa_kuichafua_chadema/2012-05-22-28</link>
			<dc:creator>twangaraha</dc:creator>
			<guid>https://siasa.ucoz.com/news/shibuda_mwana_ccm_aliye_tumwa_kuichafua_chadema/2012-05-22-28</guid>
			<pubDate>Mon, 21 May 2012 21:22:42 GMT</pubDate>
		</item>
		<item>
			<title>wizi sasa umehamia idara ya uhamiaji</title>
			<description>KASHFA nyingine imeibuliwa katika Idara ya Uhamiaji.Taarifa mpya 
yenye kurasa tano, imewataja vigogo hao saba wakidaiwa kuwa na utajiri 
wa kutisha.Taarifa hiyo ambayo tunayo nakala yake, imedai kuwa vigogo 
hao wanamiliki mali na mamilioni ya shilingi katika akaunti zao binafsi.&lt;p&gt;Maofisa
 saba wametajwa kwa majina na vituo vyao vya kazi ambavyo ni Lindi, Dar 
es Salaam, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) na Moshi.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Tuhuma
 hizo zimekuja wakati Tume Maalumu iliyoundwa kuchunguza tuhuma za 
ufisadi na utoaji wa vibali bandia kwa wageni, ikitajwa kuanza kazi 
juzi. Hata hivyo, habari kutoka wizarani zinaeleza kuwa timu hiyo 
itaanza rasmi kazi zake leo.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Habari za uhakika kutoka ndani ya 
Uhamiaji, zimedai kuwa baadhi ya wajumbe wa tume hiyo wamemhoji meneja 
wa benki moja kubwa ya Moshi ili kupata ukweli wa madai kuwa kigogo 
mmoja wa Uhamiaji mwenye cheo cha Naibu Kamishna (DCI), anamiliki 
akaunti ya fedha za kigeni.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Kigogo huyo anahusishwa pia na mtan...</description>
			<content:encoded>KASHFA nyingine imeibuliwa katika Idara ya Uhamiaji.Taarifa mpya 
yenye kurasa tano, imewataja vigogo hao saba wakidaiwa kuwa na utajiri 
wa kutisha.Taarifa hiyo ambayo tunayo nakala yake, imedai kuwa vigogo 
hao wanamiliki mali na mamilioni ya shilingi katika akaunti zao binafsi.&lt;p&gt;Maofisa
 saba wametajwa kwa majina na vituo vyao vya kazi ambavyo ni Lindi, Dar 
es Salaam, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) na Moshi.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Tuhuma
 hizo zimekuja wakati Tume Maalumu iliyoundwa kuchunguza tuhuma za 
ufisadi na utoaji wa vibali bandia kwa wageni, ikitajwa kuanza kazi 
juzi. Hata hivyo, habari kutoka wizarani zinaeleza kuwa timu hiyo 
itaanza rasmi kazi zake leo.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Habari za uhakika kutoka ndani ya 
Uhamiaji, zimedai kuwa baadhi ya wajumbe wa tume hiyo wamemhoji meneja 
wa benki moja kubwa ya Moshi ili kupata ukweli wa madai kuwa kigogo 
mmoja wa Uhamiaji mwenye cheo cha Naibu Kamishna (DCI), anamiliki 
akaunti ya fedha za kigeni.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Kigogo huyo anahusishwa pia na mtandao
 wa utoaji vibali bandia kwa raia wa kigeni wanaofanya kazi mkoani 
Kilimanjaro au kufanya kazi za kujitolea.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Ripoti hiyo imetaja 
taasisi 13, zikiwamo zisizo za kiserikali (NGO), hospitali na hoteli za 
kitalii zinazodaiwa wageni wake walipewa vibali bandia.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Mbali na 
kumhoji meneja huyo, inadaiwa pia walifanya mahojiano na uongozi wa 
kiwanda kimoja kinachodaiwa kukutwa na vibali bandia vya wageni 84.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Taarifa
 hizo zilidai kuwa maofisa wengine waandamizi wa Uhamiaji kutoka Makao 
Makuu, Dar es Salaam walitarajiwa kuwasili Moshi juzi kuungana na 
wenzao.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Baadhi ya maofisa waliotajwa katika ripoti hiyo kwamba 
wana utajiri ni wale waliokumbwa na uhamisho katika idara hiyo, Kia 
miezi mitatu iliyopita.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Katika ripoti hiyo, kigogo mmoja mwenye 
cheo cha DCI anadaiwa kukutwa na Sh700 milioni katika akaunti yake, 
achilia mbali kumiliki mali za mamilioni.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Mbali na maofisa hao 
kumiliki mamilioni ya fedha taslimu, pia wanadaiwa ‘kufanya kufuru’ ya 
kununua magari ya kifahari, nyumba na viwanja.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Ripoti hiyo 
inayodaiwa kuandikwa na Maofisa Uhamiaji wazalendo, imepinga hatua ya 
kuhamishwa kutoka kituo kimoja kwenda kingine, maofisa wanaotuhumiwa 
kukutwa na utajiri ambao haulingani na vipato vyao.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;&quot;Tunataka 
ufanyike ukaguzi wa kina wa vibali vyote vilivyotolewa kati ya 
2009/2010, 2010/2011 hadi 2012 na taasisi zote zionyeshe nakala za 
vibali,” imedai.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Pia taarifa hiyo imependekeza wenzao wote 
wanaotuhumiwa kuwa na utajiri wa kutisha wachunguzwe na Taasisi ya 
Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).&lt;/p&gt;&lt;p&gt;&quot;Haikuwa sahihi kuwahamisha na kuishia hapo, walipaswa wapelekwe Takukuru wachunguzwe chanzo cha utajiri wao.”&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Pia
 wametaka kigogo anayemiliki akaunti ya Dola, achunguzwe ili kujua 
alikuwa akifanya biashara gani nje ya utumishi wa umma na kama alilipa 
kodi kiasi gani.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Baadhi ya maofisa Uhamiaji wamependekeza 
kusimamishwa kazi kwa kigogo huyo katika kipindi hiki kwa hofu ya 
kuingilia na kuvuruga uchunguzi.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Wiki iliyopita, Kamishna Mkuu wa 
Uhamiaji, Magnus Ulungi aliwaambia waandishi wa habari kuwa imeundwa kwa
 tume ya kumchunguza kigogo huyo.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Hata hivyo, taarifa 
zilizopatikana jana zilisema tume hiyo imepanua wigo wa uchunguzi juu ya
 kuwapo kwa vibali bandia katika taasisi mbalimbali.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Kabla ya 
kuhamishiwa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, aliyekuwa Waziri
 wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Naodha alikaririwa akisema Kilimanjaro 
ni moja kati ya mikoa minane inayomtia kichefuchefu nchini.&lt;br&gt;Waziri 
huyo alisema baadhi ya watumishi wamekuwa wakijihusisha na mtandao wa 
uingiaji wahamiaji haramu nchini pia kutoa vibali bandia kwa wageni.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alipoulizwa juzi kuhusu 
sakata hilo alisema ni vyema Uhamiaji ikapewa nafasi ya kuchunguza suala
 hilo kwa kuwa tayari imeshateua tume ya uchunguzi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Kamishna 
Mkuu wa Uhamiaji tayari amelifanyia kazi jambo hilo kwa uzito 
unaostahili. Tuwape nafasi walichunguze si vyema kuanza kuingilia katika
 hatua hii ya mwanzo,” alisema.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&lt;strong&gt;Wahamiaji haramu&lt;/strong&gt;&lt;br&gt;Serikali,
 bila mafanikio, imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kukomesha tatizo la 
wahamiaji haramu linalotajwa kuwa chanzo cha utajiri wa baadhi ya vigogo
 wa Idara ya Uhamiaji.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Miongoni mwa mikakati iliyowahi kutangazwa 
na Wizara ya Mambo ya Ndani ni pamoja na idara hiyo kufanya utafiti kwa 
kushirikiana na Chuo Kikuu cha Mzumbe kubaini chanzo cha ongezeko la 
wahamiaji haramu nchini.&lt;br&gt;Akiwasilisha Bajeti ya Wizara yake bungeni 
mwaka 2007/2008 , aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wakati huo,
 Joseph Mungai alisema matokeo ya utafiti huo ni kuisaidia Serikali 
kujua chanzo cha tatizo hilo na jinsi ya kupambana nalo kwa ufanisi 
zaidi.&lt;/p&gt;&lt;p&gt;Hatua nyingine zinazochukuliwa ni pamoja na maofisa 
Uhamiaji kushiriki katika vikao mbalimbali kuanzia ngazi ya vijiji, ili 
kuwapa wananchi elimu juu ya masuala yanayohusu uraia na jinsi ya 
kukabiliana na wahamiaji haramu; Kutoa elimu kwa umma kupitia vyombo vya
 habari;&amp;nbsp;Kuweka mtandao wa kompyuta katika vituo vyote vya Uhamiaji ili 
kuviunganisha na makao makuu.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Pamoja na Serikali kutangaza 
mkakati huo miaka mitano iliyopita, wahamiaji haramu limeendelea kuwa 
tatizo sugu linalotia doa utendaji wa idara hiyo.&lt;/p&gt;</content:encoded>
			<link>https://siasa.ucoz.com/news/wizi_sasa_umehamia_idara_ya_uhamiaji/2012-05-22-27</link>
			<dc:creator>twangaraha</dc:creator>
			<guid>https://siasa.ucoz.com/news/wizi_sasa_umehamia_idara_ya_uhamiaji/2012-05-22-27</guid>
			<pubDate>Mon, 21 May 2012 21:07:09 GMT</pubDate>
		</item>
		<item>
			<title>poleni sana CCM huu ndio mwisho wenu</title>
			<description>mwalimu nyerere ambaye ndiye mwasisi wa chama cha mapinduzi aliwahi kukitabilia kifo chama ambacho yeye aliki asisi kwa madai kua kina kanza ya uongozi hebu tupate nukuu ya maneno yake kabla htuja endelea&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mwaka 1993 Mwalimu alichapisha kitabu kiitwacho Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (Harare: Zimbabwe Publishing House, 1993). Pamoja na mambo mengine katika kitabu hiki, Mwalimu alisema kuwa kuna kansa katika uongozi wa CCM. Nanukuu baadhi ya maneno yake:&lt;br&gt; &lt;br&gt;&lt;span class=&quot;text_exposed_hide&quot;&gt;...&lt;/span&gt;&lt;span class=&quot;text_exposed_show&quot;&gt; Chama cha Mapinduzi, kwa sababu ya uzito wa historia yake, hadhi ya jina lake, mfumo wa wavu wake, mazoea ya watu, na ubovu wa Vyama vya Upinzani, kinaweza kuchaguliwa na Watanzania, pamoja na kansa ya uongozi wake. Au watu wanaweza wakachoka, wakasema, &quot;potelea mbali:&quot; wakachagua Chama cho chote, ilimradi tu watokane na kansa ya uongozi wa CCM. Hainifurahishi kuyasema haya, lakini uhai wa Nchi yetu unataka yasemwe. (Ukurasa 61)&lt;br&gt; &lt;br&gt; Mwalimu...</description>
			<content:encoded>mwalimu nyerere ambaye ndiye mwasisi wa chama cha mapinduzi aliwahi kukitabilia kifo chama ambacho yeye aliki asisi kwa madai kua kina kanza ya uongozi hebu tupate nukuu ya maneno yake kabla htuja endelea&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mwaka 1993 Mwalimu alichapisha kitabu kiitwacho Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (Harare: Zimbabwe Publishing House, 1993). Pamoja na mambo mengine katika kitabu hiki, Mwalimu alisema kuwa kuna kansa katika uongozi wa CCM. Nanukuu baadhi ya maneno yake:&lt;br&gt; &lt;br&gt;&lt;span class=&quot;text_exposed_hide&quot;&gt;...&lt;/span&gt;&lt;span class=&quot;text_exposed_show&quot;&gt; Chama cha Mapinduzi, kwa sababu ya uzito wa historia yake, hadhi ya jina lake, mfumo wa wavu wake, mazoea ya watu, na ubovu wa Vyama vya Upinzani, kinaweza kuchaguliwa na Watanzania, pamoja na kansa ya uongozi wake. Au watu wanaweza wakachoka, wakasema, &quot;potelea mbali:&quot; wakachagua Chama cho chote, ilimradi tu watokane na kansa ya uongozi wa CCM. Hainifurahishi kuyasema haya, lakini uhai wa Nchi yetu unataka yasemwe. (Ukurasa 61)&lt;br&gt; &lt;br&gt; Mwalimu hakuishia hapo, bali aliongezea namna hii:&lt;br&gt; &lt;br&gt; Nilisema awali kwamba kansa ya uongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona Chama kizuri cha upinzani kinachoweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM. Ubovu wa uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa Vyama Vingi. Nilitumaini kuwa tunaweza kupata Chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM; au ambacho kingekilazimisha Chama cha Mapinduzi kusafisha uongozi wake, kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao. Lakini bado sijakiona Chama makini cha upinzani; na wala dalili zo zote za kuondoa kansa ya uongozi ndani ya CCM. Bila upinzani mzuri wa nje, na bila demokrasia halisi ndani ya Chama cha Mapinduzi, Chama hiki kitazidi kudidimia chini ya uzito wa uongozi mbovu. Kwa hali yetu ya kisiasa ilivyo nchini hili si jambo la kutarajia bila hofu na wasi wasi!(Ukurasa 66)&lt;br&gt;&lt;br&gt;miaka 19 baada ya mwalimu kusema hayo ameibuka kada mwingine wa chama hicho akiwa na madai sawa na ya mwalimu licha ya yeye mwenyewew kuwa badio sio mtu safi kwenye macho ya watanzania&lt;br&gt;&lt;br&gt;sasa hali imekuwa mbaya ndani ya ccm badala ya kujadili wafanye nini kukinusuru chama sasa wanajadili na kukosoa vibaya mapungufu makubwa waliyo nayo makada wake licha ya kukili kuwa kasi ya peoples pwa inawabana koo &lt;br&gt;&lt;br&gt;&lt;br&gt;&lt;br&gt;&amp;nbsp;&amp;nbsp; huo ndio mwisho wenu ndugu zangu wa ccm&lt;br&gt;&lt;/span&gt;</content:encoded>
			<link>https://siasa.ucoz.com/news/poleni_sana_ccm_huu_ndio_mwisho_wenu/2012-05-17-26</link>
			<dc:creator>twangaraha</dc:creator>
			<guid>https://siasa.ucoz.com/news/poleni_sana_ccm_huu_ndio_mwisho_wenu/2012-05-17-26</guid>
			<pubDate>Wed, 16 May 2012 22:37:25 GMT</pubDate>
		</item>
		<item>
			<title>Mzee Makamba awarushia kombora Nape, Pinda</title>
			<description>&lt;span style=&quot;font-family: Century Gothic; font-size: 8pt;&quot;&gt;&lt;b&gt;&lt;br&gt;&lt;/b&gt;&lt;/span&gt;&lt;h6 class=&quot;uiStreamMessage&quot;&gt;&lt;span style=&quot;font-family: Arial Black; font-size: 10pt;&quot; class=&quot;messageBody&quot;&gt;&lt;strong&gt;ASEMA NAPE ANAIGEUZA CCM MALI YAKE,PINDA YUKO MBALI NA WANANCHI, KINGUNGE PIA ACHARUKA&lt;/strong&gt;&lt;br&gt;Midraji Ibrahim, Dodoma&lt;br&gt;BAADA
 ya ukimya wa muda mrefu, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Yusuf Makamba 
ameibuka katika kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho (Nec) na 
kumtuhumu Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kwamba amekigeuza 
chama kuwa mali yake binafsi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Taarifa kutoka ndani ya kikao 
hicho, zimesema kwamba Makamba alisema hatua ya Nape kugeuza chama hicho
 kama taasisi yake binafsi ndiyo ambayo imesababisha kikose mwelekeo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Makamba
 licha ya kuelekeza mashambulizi yake kwa Nape, alimrushia pia kombora 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuwa ana uhusiano mdogo na wananchi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Mzee
 (Makamba) amesema hivi sasa CCM imekuwa kama jogoo anayepelekwa kwa 
mganga, kila anakoelekezwa ...</description>
			<content:encoded>&lt;span style=&quot;font-family: Century Gothic; font-size: 8pt;&quot;&gt;&lt;b&gt;&lt;br&gt;&lt;/b&gt;&lt;/span&gt;&lt;h6 class=&quot;uiStreamMessage&quot;&gt;&lt;span style=&quot;font-family: Arial Black; font-size: 10pt;&quot; class=&quot;messageBody&quot;&gt;&lt;strong&gt;ASEMA NAPE ANAIGEUZA CCM MALI YAKE,PINDA YUKO MBALI NA WANANCHI, KINGUNGE PIA ACHARUKA&lt;/strong&gt;&lt;br&gt;Midraji Ibrahim, Dodoma&lt;br&gt;BAADA
 ya ukimya wa muda mrefu, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Yusuf Makamba 
ameibuka katika kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho (Nec) na 
kumtuhumu Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kwamba amekigeuza 
chama kuwa mali yake binafsi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Taarifa kutoka ndani ya kikao 
hicho, zimesema kwamba Makamba alisema hatua ya Nape kugeuza chama hicho
 kama taasisi yake binafsi ndiyo ambayo imesababisha kikose mwelekeo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Makamba
 licha ya kuelekeza mashambulizi yake kwa Nape, alimrushia pia kombora 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuwa ana uhusiano mdogo na wananchi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Mzee
 (Makamba) amesema hivi sasa CCM imekuwa kama jogoo anayepelekwa kwa 
mganga, kila anakoelekezwa ndo huko, hali hiyo ndiyo inakikumba CCM hivi
 sasa. Amemweleza Nape kuwa amegeuza chama kama mali yake binafsi, 
anafanya mambo nje ya utaratibu na anaangaliwa tu.”&lt;br&gt;&lt;br&gt;Makamba 
alidai kuwa badala ya sekretarieti kushughulikia matatizo ya chama, 
imekuwa ikihangaika na watu kwa sababu ya kutofautiana nao misimamo na 
wakati huo wakijidai kuzika tofauti ili kukiimarisha.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Nape alipoulizwa kuhusu suala hilo alipuuza na kusema: &quot;Si kweli, lakini ninyi andikeni tu maana tumewazoea.”&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alipotakiwa
 kueleza kama Kingunge na Makamba walisema nini dhidi yake katika kikao 
cha Nec alijibu: &quot;Walikuwapo, lakini hakuna kati yao aliyenitaja hata 
kwa jina.”&lt;br&gt;&lt;br&gt;Nape alitumia muda mwingi kulalamika kuwa taarifa 
nyingi ambazo zimekuwa zikitolewa kutoka ndani ya mkutano huo 
uliomalizika jana zimetoka kwa watu aliowataja kuwa wana maslahi nazo 
binafsi na kuhoji,” Kwa nini msiwe mnasubiri taarifa rasmi (za chama) 
ili habari iwe ya ukweli zaidi?”&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mkongwe mwingine wa chama hicho,
 Kingunge Ngombale-Mwiru, ambaye anadaiwa kusikitishwa na vitendo vya 
rushwa na ugomvi vinavyoendelea ndani ya chama huku vikiangaliwa na 
viongozi kama vile vinakistawisha wakati vinakiporomosha.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kingunge
 alidai kuwa hivi sasa chama hicho kimetawaliwa na matajiri ambao ndiyo 
wanaopata nafasi za uongozi na maskini wanawekwa kando.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mwenyekiti
 wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja aliunga mkono suala la Pinda kuwa
 na uhusiano mdogo na wananchi na kwamba, amekuwa mkimya zaidi na 
hamsaidii Rais Jakaya Kikwete.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Yule Mwenyekiti wa Shinyanga, 
amemweleza Pinda kuwa ng’ombe wakila mazao mtu wa kwanza kuchapwa viboko
 ni mchungaji, halafu mmiliki anatozwa faini baadaye. Hivyo, alitakiwa 
kuwajibika kwanza kabla ya mawaziri walioondolewa,” kilidokeza chanzo 
chetu.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mgeja alidai kuwa uwajibishwaji wa mawaziri, haukuzingatia
 haki kwa sababu George Mkuchika, Profesa Jumanne Maghembe na Hawa 
Ghasia walilalamikiwa, lakini kilichofanywa ni kutoa kafara wengine na 
hao kubadilishiwa wizara.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Pia, inadaiwa kuwa Mwenyekiti Kikwete 
aliwataka wajumbe kuzika tofauti zao ili kuweka msimamo wa pamoja kwa 
ajili ya ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu ujao wa 2015 na kwamba adui namba 
moja wa CCM hivi sasa ni Chadema.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Rushwa yakishtua chama&lt;br&gt;&lt;br&gt;Katibu
 wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema Nec imejadili changamoto 
zinazokikabili chama kwenye uchaguzi unaoendelea na kubaini kuwa rushwa 
imekithiri.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Nape alisema tishio la rushwa ni kubwa na mgombea 
atayakayethibitika kujihusisha na vitendo hivyo rushwa ataondolewa mara 
moja, huku viongozi na watendaji wakitahadharishwa kuchukuliwa hatua za 
nidhamu.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Kwa kisingizio cha kuwasalimia wajumbe, kuwapa nauli au
 kujitambulisha. Mgombea atakayethibitika anazunguka au amezunguka 
ataondolewa bila kuchelewa katika orodha ya wagombea,” alisema na 
kuongeza:&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Kwa watendaji na viongozi wa chama ngazi zote kuanzia 
sasa ni marufuku kuwatembeza ndani ya maeneo yao, kwa nia ya 
kuwatambulisha kwa wapiga kura. Mtendaji au kiongozi atakayebainika 
anakiuka agizo hili, atachukuliwa hatua za nidhamu mara moja.”&lt;br&gt;&lt;br&gt;Pia,
 Nape alisema kuanzia sasa ni marufuku kwa watendaji na viongozi wa 
chama ngazi zote kuwaitia wagombea, wajumbe wa mikutano ya uchaguzi kwa 
lengo lolote, kwani vikao vya aina hiyo havimo katika katiba.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alisema
 vikao vya aina hiyo ni haramu na vinapalilia rushwa na kuongeza kwamba 
wanachama wa CCM wanatakiwa kupiga vita rushwa na kutoa taarifa ya 
vitendo hivyo katika ofisi za chama na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na
 Rushwa (Takukuru).&lt;br&gt;&lt;br&gt;Aliitaka Takukuru kutomuonea aibu au kumuogopa mtu anayejihusisha na vitendo vya rushwa badala yake wamchukulie hatua.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mishahara na chakula&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kuhusu
 mishahara ya watumishi wa umma na mfumuko wa bei ya chakula, Nape 
alisema Nec imeagiza Serikali kuhimiza waajiri kupandisha mishahara na 
malipo mengine kwa wafanyakazi wao ili waweze kumudu gharama za maisha.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alisema
 gharama za maisha zimepanda na mishahara inayolipwa haiendani na hali 
halisi. Alisema nayo Serikali inatakiwa nayo kupandisha mishahara kwa 
watumishi wake.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Serikali idhibiti malipo ya huduma ya ndani kwa 
kutumia fedha za kigeni, hasa Dola ya Marekani. Pia, iongeze udhibiti wa
 maduka na hoteli zinazofanya biashara ya fedha za kigeni ili kuondoa 
hujuma kwa uchumi wa nchi inayofanywa kutokana na uhuru uliokithiri 
katika biashara hii,” alisema.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Nape alisema Serikali inatakiwa 
kuweka jitihada zaidi za kudhibiti ulanguzi wa bidhaa muhimu na 
upandishaji holela wa bei za vyakula, kodi za nyumba na usafiri.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alisema Nec imeagiza Serikali kuendelea kuchukua hatua za muda mrefu na kati za kukabiliana na tatizo la mfumuko wa bei.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;CCM
 inaiagiza Serikali kuchukua hatua za haraka na muda mfupi ikiwamo 
kuangalia upya baadhi ya kodi katika vyakula pamoja na Kodi ya Ongezeko 
la Thamani (VAT) katika sukari,” alisema Nape.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Pia, Nape alisema 
wameagiza Serikali kupitia upya utaratibu wa ruzuku ya mbegu na mbolea 
ili upanuliwe kunufaisha wakulima wengi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alisema Nec imeitaka 
Serikali iongeze kasi ya utekelezaji wa mpango wake wa kuongeza uwezo wa
 kuhifadhi chakula nchini, hasa kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Nafaka ya 
Taifa (NFRA), ikiwamo kujenga maghala zaidi ya mazao ya chakula maeneo 
ya uzalishaji na kutenga fedha nyingi zaidi kwa ununuzi wa mazao hayo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Wakati
 wa uhaba wa vyakula maeneo ya mijini, kasi ya kupeleka chakula maeneo 
hayo iongezwe na utaratibu mzuri zaidi wa usambazaji chakula utumike ili
 walaji na siyo wasafirishaji na wasindikaji, wanufaike,” alisema.&lt;/span&gt;&lt;/h6&gt;source mwananchi&lt;br&gt;&lt;br&gt;</content:encoded>
			<link>https://siasa.ucoz.com/news/2012-05-17-25</link>
			<dc:creator>twangaraha</dc:creator>
			<guid>https://siasa.ucoz.com/news/2012-05-17-25</guid>
			<pubDate>Wed, 16 May 2012 22:15:59 GMT</pubDate>
		</item>
		<item>
			<title>mambo yaenda vibaya,ikulu yapingwa</title>
			<description>WANAHARAKATI nchini wamepinga&amp;nbsp;&amp;nbsp; mpango wa Ikulu wa kutaka kuwapo na 
uchunguzi wa watendaji katika wizara na taasisi nyingine za umma 
wanaotuhumiwa kuhusika na ubadhirifu wa fedha za umma kwa kigezo kwamba 
ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inatosha 
kuwafikisha mahakamani.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kauli hiyo imekuja baada ya juzi Ikulu&amp;nbsp; 
kuagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na 
Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) kuwachunguza watendaji hao na kwamba
 uchunguzi huo kwa kile walichoeleza ni ili kutomuonea mtu wala 
kukandamiza wakati wa kuchukua hatua.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wakichangia maoni katika 
mada ya hali ya uwajibikaji nchini iliyotolewa kwenye Semina ya 
Maendeleo na Jinsia (GDSS), iliyofanyika katika viwanja vya Mtandao wa 
Jinsia Tanzania (TGNP) jijini Dar es Salaam walisema , tuhuma 
zilizowaondoa kwenye nafasi zao ni za kushindwa kuwajibika na si za 
rushwa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Jinsia katika mtandao huo, 
Diana Mwiru alisema...</description>
			<content:encoded>WANAHARAKATI nchini wamepinga&amp;nbsp;&amp;nbsp; mpango wa Ikulu wa kutaka kuwapo na 
uchunguzi wa watendaji katika wizara na taasisi nyingine za umma 
wanaotuhumiwa kuhusika na ubadhirifu wa fedha za umma kwa kigezo kwamba 
ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inatosha 
kuwafikisha mahakamani.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kauli hiyo imekuja baada ya juzi Ikulu&amp;nbsp; 
kuagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na 
Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) kuwachunguza watendaji hao na kwamba
 uchunguzi huo kwa kile walichoeleza ni ili kutomuonea mtu wala 
kukandamiza wakati wa kuchukua hatua.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wakichangia maoni katika 
mada ya hali ya uwajibikaji nchini iliyotolewa kwenye Semina ya 
Maendeleo na Jinsia (GDSS), iliyofanyika katika viwanja vya Mtandao wa 
Jinsia Tanzania (TGNP) jijini Dar es Salaam walisema , tuhuma 
zilizowaondoa kwenye nafasi zao ni za kushindwa kuwajibika na si za 
rushwa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Jinsia katika mtandao huo, 
Diana Mwiru alisema kwa sasa hakuna haja ya kufanya uchunguzi kwa kuwa 
ripoti ya CAG na zile za kamati tatu za Bunge zinaonyesha wazi namna 
wahusika walivyohusika katika tuhuma hizo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Tuhuma zinazowahusu 
mawaziri zinatokana na wao kushindwa kuwajibika na kulisababishia hasara
 taifa, … ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za serikali (CAG) na ripoti za 
kamati tatu za Bunge zote&amp;nbsp; ziko wazi na wote tumeona hasara iliyotokea 
,hoja yangu ni kwamba tunachunguza nini tena? alihoji Mwiru na kuongeza:&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Kinachotakiwa
 kwa sasa ni&amp;nbsp; wahusika kufikisha mahakamani kujibu tuhuma, unafanyika 
uchunguzi mwingine wa nini, hawa wanatufanya sisi hatujui kitu, kazi ya 
Takukuru ni kuchunguza rushwa swali ni je tuhuma hizo ni za rushwa? 
alihoji Mwiru.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mwiru alisisitiza kuwa chunguzi zilizofanywa 
zinatosha na sasa Watanzania wanataka kuona watuhumiwa wakifikishwa 
kwenye mhimili mwingine unaotafsiri sheria (Mahakama) ili kuona haki 
inatendeka.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mawaziri waliondolewa katika nafasi zao walitajwa
 katika ripoti ya CAG, na pia ripoti za kamati za kudumu za Bunge 
zilizowasilishwa kwenye vikao vya Bunge lilifanyika hivi karibuni mkoani
 Dodoma.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kamati hizo ni ile ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za 
Serikali na Mashirika ya Umma (POAC) ambayo Mwenyekiti wake ni Mbunge wa
 Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na
 Mazingira&amp;nbsp; Mwenyekiti wake , James Lembeli zilionyesha namna mawaziri 
walivyoshindwa kuwajibika na kusababishia taifa hasara kubwa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Ripoti
 za kamati hizo bungeni ziliibua tuhuma za upotevu wa fedha huku 
zikiwataja baadhi ya mawaziri kushindwa kuwajibika hali iliyomsukuma 
Mbunge wa Kigoma kaskazini, Zitto Kabwe kuitisha hoja ya kukusanya saini
 za kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Akitoa
 mada katika washa hiyo, Amina Uddy mwanaharakati kutoka ForDIA, alisema
 hali ya uwajibikaji nchini imeshuka&amp;nbsp; kwa kiwango kikubwa hali 
inayowafanya viongozi washindwe kujali na kusimamia rasilimali za umma.</content:encoded>
			<link>https://siasa.ucoz.com/news/mambo_yaenda_vibaya_ikulu_yapingwa/2012-05-13-24</link>
			<dc:creator>twangaraha</dc:creator>
			<guid>https://siasa.ucoz.com/news/mambo_yaenda_vibaya_ikulu_yapingwa/2012-05-13-24</guid>
			<pubDate>Sun, 13 May 2012 07:31:39 GMT</pubDate>
		</item>
		<item>
			<title>Sugu aelekea Ruvuma kuvuna wanachama</title>
			<description>&lt;div class=&quot;text1&quot;&gt;
 &lt;p&gt;MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), leo anatarajiwa kuanza ziara ya kukijenga chama Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu kutoka Mbeya, Sugu
 alisema kuwa anaanza ziara ya kichama ya siku tatu mkoani Ruvuma, 
ambako atahutubia mikutano ya hadhara.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Mbilinyi maarufu kama ‘Sugu’ alisema kuwa leo atafanya mkutano huko 
Madaba na kesho atakuwa mji mdogo wa Mbinga na Jumapili atamalizia mjini
 Songea.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 &quot;Leo nitaanza ziara ya siku tatu ya kichama mkoani Ruvuma, ambako 
nitaungana na viongozi wengine wa Chachema mkoani humo, kuhutubia 
mikutano ya hadhara ili kusaka wananchama wapya kutoka Nyanda za Juu 
Kusini,” alisema Sugu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Katika hatua nyingine, Sugu alisema kuwa anashukuru kuona ujenzi wa 
barabara kwa kiwango cha lami katikati ya mji wa Mbeya unaendelea 
vizuri, jambo linalompa faraja kwamba anatekeleza ahadi zake za 
kuwaletea maendeleo wakazi wa Mbeya.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Alisema ...</description>
			<content:encoded>&lt;div class=&quot;text1&quot;&gt;
 &lt;p&gt;MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), leo anatarajiwa kuanza ziara ya kukijenga chama Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu kutoka Mbeya, Sugu
 alisema kuwa anaanza ziara ya kichama ya siku tatu mkoani Ruvuma, 
ambako atahutubia mikutano ya hadhara.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Mbilinyi maarufu kama ‘Sugu’ alisema kuwa leo atafanya mkutano huko 
Madaba na kesho atakuwa mji mdogo wa Mbinga na Jumapili atamalizia mjini
 Songea.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 &quot;Leo nitaanza ziara ya siku tatu ya kichama mkoani Ruvuma, ambako 
nitaungana na viongozi wengine wa Chachema mkoani humo, kuhutubia 
mikutano ya hadhara ili kusaka wananchama wapya kutoka Nyanda za Juu 
Kusini,” alisema Sugu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Katika hatua nyingine, Sugu alisema kuwa anashukuru kuona ujenzi wa 
barabara kwa kiwango cha lami katikati ya mji wa Mbeya unaendelea 
vizuri, jambo linalompa faraja kwamba anatekeleza ahadi zake za 
kuwaletea maendeleo wakazi wa Mbeya.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Alisema kuwa anaamini ataweza kuzitimiza ahadi zake zote ndani ya muda
 muafaka kutokana na jinsi wananchi na watendaji wa Mbeya wanavyomuunga 
mkono.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 &quot;Kwa kweli ninafarijika kuona wananchi wa Mbeya pamoja na watendaji wa
 serikali wanaweka itikadi pembeni na wanakuwa na lugha moja katika 
kutekeleza miradi ya maendeleo,” alisisitiza Sugu.&lt;/p&gt;
 &lt;/div&gt;</content:encoded>
			<link>https://siasa.ucoz.com/news/sugu_aelekea_ruvuma_kuvuna_wanachama/2012-05-11-23</link>
			<dc:creator>twangaraha</dc:creator>
			<guid>https://siasa.ucoz.com/news/sugu_aelekea_ruvuma_kuvuna_wanachama/2012-05-11-23</guid>
			<pubDate>Fri, 11 May 2012 07:06:10 GMT</pubDate>
		</item>
		<item>
			<title>nasari afunguka kwa waandishi wa habari</title>
			<description>&lt;div class=&quot;text1&quot;&gt;&lt;p&gt;MBUNGE wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (CHADEMA), amesema kuwa 
hana nia wala dhamira ya kuchochea na kuhamasisha mgawanyiko katika nchi
 kama ambavyo imekuwa ikitafsiriwa na baadhi ya watu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Akizungumza na waandishi wa habari jana, juu ya maneno anayodaiwa 
kuyatoa Jumamosi kwenye mkutano wa hadhara wa chama chake wakati wa 
uzinduzi wa operesheni ‘vua gamba vaa gwanda’ kwenye viwanja vya NMC, 
Nassari alidai lengo la hotuba yake lilikuwa kuhimiza serikali na jeshi 
la polisi lishughulikie mauaji ya watu na kudai hakulenga kuchochea 
vurugu au kumzuia Rais kutekeleza wajibu wake.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 &quot;Kumetokea sintofahamu kubwa kuhusu sehemu ya hotuba yangu niliyoitoa;
 chama changu siku zote kimekuwa mstari wa mbele kuunganisha umma wa 
Watanzania wote kudai haki, umoja, amani na maendeleo ya kweli bila 
kujali ukanda, udini wala historia, ningependa ifahamike kuwa sina lengo
 wala dhamira ya kuwagawa Watanzania kwa namna yoyote ile kama ambavyo 
imekuwa ikita...</description>
			<content:encoded>&lt;div class=&quot;text1&quot;&gt;&lt;p&gt;MBUNGE wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (CHADEMA), amesema kuwa 
hana nia wala dhamira ya kuchochea na kuhamasisha mgawanyiko katika nchi
 kama ambavyo imekuwa ikitafsiriwa na baadhi ya watu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Akizungumza na waandishi wa habari jana, juu ya maneno anayodaiwa 
kuyatoa Jumamosi kwenye mkutano wa hadhara wa chama chake wakati wa 
uzinduzi wa operesheni ‘vua gamba vaa gwanda’ kwenye viwanja vya NMC, 
Nassari alidai lengo la hotuba yake lilikuwa kuhimiza serikali na jeshi 
la polisi lishughulikie mauaji ya watu na kudai hakulenga kuchochea 
vurugu au kumzuia Rais kutekeleza wajibu wake.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 &quot;Kumetokea sintofahamu kubwa kuhusu sehemu ya hotuba yangu niliyoitoa;
 chama changu siku zote kimekuwa mstari wa mbele kuunganisha umma wa 
Watanzania wote kudai haki, umoja, amani na maendeleo ya kweli bila 
kujali ukanda, udini wala historia, ningependa ifahamike kuwa sina lengo
 wala dhamira ya kuwagawa Watanzania kwa namna yoyote ile kama ambavyo 
imekuwa ikitafsiriwa,” alisema Nasari.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Alisema hata kauli ya ufafanuzi iliyotolewa na Mwenyekiti wake wa 
Taifa, Freeman Mbowe, kwenye mkutano huo baada ya yeye kuzungumza 
iliweka mkazo juu ya msimamo wa CHADEMA wa kuunganisha nguvu ya umma 
katika maendeleo ya Watanzania.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 &quot;Hata alipohojiwa na vyombo vya usalama kutaka kujua nilimaanisha nini aliwaeleza hivyo,” alisema.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Nassari ametoa kauli hiyo siku moja baada ya jeshi la polisi kudai 
linasubiri ridhaa ya Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) ili waweze 
kumfikisha mahakamani pamoja Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa, John Heche, na
 mwanachama Ally Bananga ambaye alikuwa amehamia CHADEMA siku hiyo ya 
mkutano akitokea CCM alikokuwa akishika nyadhifa mbalimbali za uongozi.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Naibu Kamishina wa Polisi, Isaya Mungulu, aliwaeleza waandishi wa 
habari juzi kuwa baada ya kuwahoji wamebaini makosa wanayowatuhumu nayo
 yanaangukia katika kifungu cha sheria namba 63 b cha kanuni ya adhabu, 
sura namba 16 ambapo inahitaji ridhaa ya DPP kabla ya kuyafikisha 
mahakamani.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;&lt;strong&gt;UVCCM wamshukia &lt;/strong&gt;&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;UMOJA wa vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) umemtaka Msajili wa 
Vyama vya Siasa nchini, kuviwajibisha baadhi ya vyama ambavyo vinatumia 
vibaya uhuru wake.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Katibu mkuu wa umoja huo, Martin Shigela, alisema hayo jana 
alipokutana na wanachama wa umoja huo kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma 
(UDOM), akidai kuwa amesikitishwa na kauli iliyotolewa hivi karibuni na 
mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari, ya kulitaka jeshi la polisi
 kuwakamata waliohusika na mauaji ya wanachama wake, vinginevyo 
wangelijitangazia uhuru wao.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Alidai kuwa kauli ya Nassari ni ya kibaguzi na yenye lengo la 
kuchochea umwagaji damu, hivyo, lazima hatua zichukuliwe dhidi ya 
viongozi wa aina hiyo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Aliwaambia wanavyuo hao walioandamano kwa ajili ya kumpongeza Rais 
Jakaya Kikwete kwa ajili ya mabadiliko ya baraza la mawaziri kuwa CCM 
inalaani kauli hiyo kwani siyo kauli nzuri katika mwenendo wa kisiasa.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Hata hivyo, wakati Shigela akilalama, tayari viongozi wa ngazi ya juu 
wa CHADEMA, wametoa maelezo kuwa huo sio msimamo wa chama chao, na 
Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, alisimama na kukemea kauli hiyo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Kwa upande wake, Nasari amedai kuwa kauli yake haikuwa na lengo baya 
na ililenga kuweka mabadiliko ya kihamasa katika mikoa hiyo ili wengine 
waone wivu wa kimaendeleo kwa mikoa ya kaskazini ambayo inaonyesha 
mabadiliko makubwa.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 &quot;Mimi ni mtu mdogo tu sina nguvu hata kidogo ya kutangaza uhuru huo wa sehemu yoyote ya nchi” alifafanua Nasari.&lt;/p&gt;&lt;/div&gt;</content:encoded>
			<link>https://siasa.ucoz.com/news/nasari_afunguka_kwa_waandishi_wa_habari/2012-05-11-22</link>
			<dc:creator>twangaraha</dc:creator>
			<guid>https://siasa.ucoz.com/news/nasari_afunguka_kwa_waandishi_wa_habari/2012-05-11-22</guid>
			<pubDate>Fri, 11 May 2012 06:53:43 GMT</pubDate>
		</item>
		<item>
			<title>CHADEMA yatishia kuiumbua CCM</title>
			<description>&lt;div class=&quot;text1&quot;&gt;
 &lt;p&gt;CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetishia kuweka 
hadharani majina ya mawaziri na wabunge ambao walikuwa tayari kujiunga 
na chama hicho.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, 
Mkurugenzi wa Uenezaji wa chama hicho, John Mnyika, alisema Chama cha 
Mapinduzi kisitake kuilazimisha CHADEMA iseme ukweli wote juu ya wimbi 
kubwa la wana CCM, wakiwemo wabunge na mawaziri ambao wanataka kujiunga 
nayo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Mnyika akijibu taarifa ya CCM iliyotolewa na Katibu wa Uenezi na 
Itikadi, Nape Nnauye, alisema kuwa viongozi wengi wa chama hicho tawala 
wanajua mchakato mzima uliokuwepo wa wabunge, mawaziri na wana CCM 
wengine kutaka kuhamia CHADEMA tangu wakati wa uchaguzi mkuu wa 2010 
lakini wakaingiliwa.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Mnyika aliwataka viongozi wa CCM waseme kama wako tayari kupokea 
ukweli mchungu wa viongozi wao walio tayari kukihama chama hicho na 
kujiunga na upinzani 
 &quot;Wasitulazimishe kusema. Na kama wanataka waseme kama wak...</description>
			<content:encoded>&lt;div class=&quot;text1&quot;&gt;
 &lt;p&gt;CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetishia kuweka 
hadharani majina ya mawaziri na wabunge ambao walikuwa tayari kujiunga 
na chama hicho.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, 
Mkurugenzi wa Uenezaji wa chama hicho, John Mnyika, alisema Chama cha 
Mapinduzi kisitake kuilazimisha CHADEMA iseme ukweli wote juu ya wimbi 
kubwa la wana CCM, wakiwemo wabunge na mawaziri ambao wanataka kujiunga 
nayo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Mnyika akijibu taarifa ya CCM iliyotolewa na Katibu wa Uenezi na 
Itikadi, Nape Nnauye, alisema kuwa viongozi wengi wa chama hicho tawala 
wanajua mchakato mzima uliokuwepo wa wabunge, mawaziri na wana CCM 
wengine kutaka kuhamia CHADEMA tangu wakati wa uchaguzi mkuu wa 2010 
lakini wakaingiliwa.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Mnyika aliwataka viongozi wa CCM waseme kama wako tayari kupokea 
ukweli mchungu wa viongozi wao walio tayari kukihama chama hicho na 
kujiunga na upinzani 
 &quot;Wasitulazimishe kusema. Na kama wanataka waseme kama wako tayari, 
tufungue boksi, ikibidi hata nitaje majina ya watu na kwa nini baadaye 
walishindwa kujiunga,” alisema Mnyika.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Mnyika alisema imekuwa ni kawaida ya CCM kukanusha kila kitu, na 
kumlinganisha Nape na aliyekuwa Waziri wa Habari wa Iraq chini ya 
utawala wa Saddam Hussein ambaye alikanusha kila kitu, huku akijua 
majeshi ya Marekani yalikuwa yamewazidi nguvu.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 &quot;Sisi hatuwashangai wao kukanusha maana hata wakati waliokuwa madiwani
 wao wanahama kutoka CCM kuja CHADEMA walikanusha hivihivi, lakini leo 
yako wapi, madiwani kuanzia Arusha mpaka Mwanza huko wamehamia CHADEMA, 
hivyo hata hili la wabunge na mawaziri atakanusha sana lakini si atulie 
asubiri aone,” amesema Mnyika.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Taarifa ya CCM iliyotolewa jana imekanusha madai yaliyotolewa na 
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe, ambaye mwishoni mwa wiki 
jana alitangaza katika mkutano mkubwa wa hadhara jijini Arusha kuwa 
wabunge 70 na mawaziri kadhaa walikuwa tayari kujiunga na chama hicho 
cha upinzani.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Nape alidai kuwa maneno hayo ya Mbowe ni uongo kwa vile hakuna waziri 
au mbunge ambaye yuko tayari kuondoka ndani ya CCM na kwamba yametolewa 
kwa lengo la kujipatia umaarufu wa bure.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;&lt;strong&gt;Hoja ya mauaji&lt;/strong&gt;&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;Akizungumzia tamko la CCM lililotolewa jana kukanusha tuhuma za 
kuhusika na mauaji, Mnyika alikishambulia vikali chama tawala akidai 
kimeshindwa, Nape anaficha ukweli juu ya kuhusika kwa baadhi ya viongozi
 wake na mauaji hayo.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 &quot;Kama angetafakari kabla ya kusema angejua kuwa mpaka sasa viongozi wa
 serikali wanaotokana na CCM wako chini ya ulinzi wa polisi kuhusiana na
 mauaji ya Mwenyekiti wa CHADEMA Kata ya Usa River. Lakini pia viongozi 
na wanachama wa CCM wametajwa kwa majina kuhusika katika tukio la 
wabunge wa CHADEMA kukatwa mapanga huko Mwanza. Na mpaka sasa wako chini
 ya uchunguzi wa Jeshi la Polisi Mwanza,” alisema Mnyika.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Aliongeza kuwa kuna majina ya viongozi wa CCM waliotajwa kuhusika 
katika vitendo vya mauaji na vingine vya utekaji kwa wanachama na makada
 wa CHADEMA katika maeneo mbalimbali mathalani wakati wa uchaguzi mdogo 
wa Kiteto, Busanda, Biharamulo na kwingine.&lt;/p&gt;
&lt;p&gt;
 Mnyika aliongeza kuwa kama kweli CCM inataka kuonyesha kuwa ina 
uchungu na inakerwa na wimbi la mauaji ya kisiasa yanayoendelea nchini, 
basi walizungumze suala hilo katika vikao vyao kuielekeza serikali 
kutumia sheria ya Inquest Act, sura ya 24 ya sheria za Tanzania ambayo 
inaitaka serikali kuchunguza vifo vyenye utata.&lt;/p&gt;
 &lt;/div&gt;</content:encoded>
			<link>https://siasa.ucoz.com/news/chadema_yatishia_kuiumbua_ccm/2012-05-11-21</link>
			<dc:creator>twangaraha</dc:creator>
			<guid>https://siasa.ucoz.com/news/chadema_yatishia_kuiumbua_ccm/2012-05-11-21</guid>
			<pubDate>Fri, 11 May 2012 06:48:09 GMT</pubDate>
		</item>
		<item>
			<title>Mawaziri waanza kwa mkwara</title>
			<description>SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kufanya mabadiliko makubwa katika
 Baraza lake la mawaziri, mawaziri na manaibu wapya wamesema 
watahakikisha wanafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na Watanzania.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Juzi
 Rais Kikwete alifanya uteuzi huo kwa kufanya mabadiliko makubwa ya 
Baraza lake kwa kuingiza sura 13 mpya huku mawaziri na naibu mawaziri 
nane wakitupwa nje ya baraza hilo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Katika mabadiliko hayo, 
amewapandisha naibu mawaziri wanne kuwa mawaziri kamili na kuwahamisha 
mawaziri nane na naibu mawaziri sita, huku mawaziri na naibu mawaziri 22
 wakibaki katika wizara zao za awali.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Dk Mgimwa&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wakizungumza
 kwa nyakati tofauti na Mwananchi Jumapili Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk
 William Mgimwa, alisema uteuzi huo ni jambo la heshima hivyo ni lazima 
kujituma na kufanya kazi kwa maslahi ya Watanzania.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alipoulizwa 
jinsi atakavyokabiliana na changamoto ndani ya wizara hiyo ikiwa ni 
pamoja na tuhuma zilizomng ‘oa aliyekuwa waziri wa wizara hiyo Mustapha 
M...</description>
			<content:encoded>SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kufanya mabadiliko makubwa katika
 Baraza lake la mawaziri, mawaziri na manaibu wapya wamesema 
watahakikisha wanafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na Watanzania.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Juzi
 Rais Kikwete alifanya uteuzi huo kwa kufanya mabadiliko makubwa ya 
Baraza lake kwa kuingiza sura 13 mpya huku mawaziri na naibu mawaziri 
nane wakitupwa nje ya baraza hilo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Katika mabadiliko hayo, 
amewapandisha naibu mawaziri wanne kuwa mawaziri kamili na kuwahamisha 
mawaziri nane na naibu mawaziri sita, huku mawaziri na naibu mawaziri 22
 wakibaki katika wizara zao za awali.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Dk Mgimwa&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wakizungumza
 kwa nyakati tofauti na Mwananchi Jumapili Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk
 William Mgimwa, alisema uteuzi huo ni jambo la heshima hivyo ni lazima 
kujituma na kufanya kazi kwa maslahi ya Watanzania.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alipoulizwa 
jinsi atakavyokabiliana na changamoto ndani ya wizara hiyo ikiwa ni 
pamoja na tuhuma zilizomng ‘oa aliyekuwa waziri wa wizara hiyo Mustapha 
Mkulo, Dk Mgimwa ambaye ni Mbunge wa Kalenga alisema kabla ya kufanya 
lolote ni lazima kujiridhisha.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Bungeni tulikuwa tunazungumza 
mengi kuhusu wizara hii lakini niseme kwamba ni lazima ufanye tathmini 
na ukishajua hali halisi ya tatizo ndio unaweza kuzungumza suluhisho la 
tatizo husika ni nini, hakuna kisichowezekana,” alisema Dk Mgimwa&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alisema
 atafanya kazi kwa kujituma na uzalendo mkubwa ili kuhakikisha makusanyo
 ya fedha yanaongezeka, matumizi ya fedha yanafanyika kama yalivyopangwa
 na&amp;nbsp; kuboresha ukusanyaji wa mapato.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Makamba&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kwa upande 
wake Naibu Waziri wa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano, 
January Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli, alisema moja ya mambo 
ya kufanya katika wizara hiyo ni kuitazama upya gharama za mitandao ya 
simu, mitandao kutofika maeneo ya vijijini pamoja na huduma hiyo kuwa 
bora zaidi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Wizara hii inagusa maisha ya kila siku ya Mtanzania 
hivyo kuna ulazima wa kutizama gharama za mitandao ya simu ili iendane 
na maisha halisi ya mtanzania” alisema Makamba.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Akizungumzia 
masuala ya sayansi, Makamba alisema kuwa kuna ulazima wa kutizama upya 
msingi wa elimu ya sayansi kuanzia shule ya msingi kwa kushirikiana na 
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi, lengo likiwa ni kuongeza idadi ya 
wanafunzi wanaosoma somo hilo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Pia, aligusia mikakati iliyowekwa 
awali ya asilimia moja ya pato la taifa kuingizwa katika ufanyaji wa 
tafiti mbalimbali na kwamba umefikia wakati wa suala hilo kuanza 
kutekelezwa kikamilifu.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Tunatakiwa kuondoa urasimu wa matumizi 
ya teknolojia, hakuna haja ya watumishi wa Serikali na wananchi kupanga 
foleni kwa ajili ya kuchukua fomu, huu ni wakati wa fomu kujazwa katika 
mitandao tu,” alisema Makamba.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Hata hivyo, Makamba alisema kuwa mambo mengi anayoyaona na kuyazungumza hata bungeni yameshaanza kufanyiwa kazi na wizara hiyo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Rashid&lt;br&gt;&lt;br&gt;Naibu
 Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Suleiman Rashid alisema kuwa
 kipaumbele katika wizara hiyo ni kuhakikisha huduma zinawafikia 
wananchi, tena kwa ubora mkubwa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Huduma ya afya inatakiwa 
kuwafikia watu wote nchini ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mgonjwa 
anasafirishwa eneo moja mpaka jingine kwa usalama” alisema Dk Rashid.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Rashid
 ambaye pia ni Mbunge wa Rufiji alisema kuwa wizara inatakiwa 
kushughulikia sera na kutengeneza mipango mizuri ili watumishi wake 
wafanye kazi katika mazingira bora kwa faida yao na Watanzania wote.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Tizeba&lt;br&gt;&lt;br&gt;Naye
 Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba ambaye ni Mbunge wa Buchosa
 alisema kwa kuwa ni msaidizi wa waziri wa wizara hiyo, Dk Harrison 
Mwakyembe, atahakikisha kila jambo analofanya bosi wake linakwenda sawa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Namshuruku
 sana Rais Kikwete, Waziri Mkuu na Makamu wa Rais kwa kuwa wao ndio 
waliopendekeza mimi kuteuliwa kuwa waziri, nitatumia elimu&amp;nbsp; yangu na 
uzoefu katika Serikali katika utendaji wangu wa kazi” alisema Dk Tizeba.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mahenge &lt;br&gt;&lt;br&gt;Kwa
 upande wake Naibu Waziri wa Wizara ya Maji, Dk Binilith Mahenge ambaye 
ni Mbunge wa Makete, alisema kuwa atazungumza zaidi mara baada ya 
kuapishwa. &lt;br&gt;&lt;br&gt;Masele&lt;br&gt;Akizungumzia kuteuliwa kwake Masele alisema
 kwanza atapambana kudhibiti mali ya umma, kuhakikisha udhibiti wa 
madini na kupata thamani halisi ya kile kinachozalishwa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Pia 
alisema atashughulikia matatizo ya wachimbaji wadogo ambao wamekuwa 
wakinyonywa ili waweze kupata haki zao stahiki na kuinua uchumi wao.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Niwahakikishie Watanzania kwamba nimepewa nafasi kubwa na nitafanya kazi kwa uadilifu,&quot;alisema Masele.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Aliongeza
 kuwa; &quot;Tutahakikisha tunazipitia sheria na kuhakikisha wamiliki wa 
migodi wanawasaidia wananchi na kila sehemu ulipo mgodi tutashughulikia 
ili wananchi na serikali vyote vinufaike.&quot;&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alisema kuna watu 
wanapotosha kuhusu elimu yake, lakini ana Shahada ya Sayansi ya Siasa na
 Uhusiano wa Kimataifa aliyoipata kutoka Chuo Kikuu cha Dar es 
Salaam(UDSM) ambako alihitimu mwaka 2004.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Pia amewahi kufanya kazi katika benki kabla ya kupata nafasi ya kuwa Meneja Kanda ya Ziwa wa Kampuni ya Simu ya Mkononi ya Tigo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mawaziri walioachwa wazungumza &lt;br&gt;&lt;br&gt;Baadhi
 ya Mawaziri waliochwa kwenye baraza la jipya, wameelezea kilicho moyoni
 mwao katika kipindi hiki ambacho sasa watahudhuria Bunge kama wabunge 
wa kawaida na watapata fursa ya kuibana Serikali kiutendaji.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mtufatakamba&lt;br&gt;&lt;br&gt;Aklizungumza
 na Mwananchi Jumapili, aliyekuwa Naibu Waziri wa Uchukuzi, Athuman 
Mfutakamba alisema: &quot;Kwanza namshukuru Mheshimiwa Rais (Jakaya Kikwete) 
kwa kuniteua kuwa Naibu Waziri, kwa kipindi chote cha miaka miwili 
nimejifunza na nimekumbana na changamoto nyingi.”&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kuhusu baraza 
lililosukwa upya, Mfutakamba alisema anampongeza Rais Kikwete kwa kuteua
 watu makini na wenye elimu kusimamia Wizara ya Uchukuzi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alisema uteuzi wa Dk Harison Mwakyembe kuwa Waziri wa Uchukuzi na Charles Tizeba kuwa naibu wake, umefanywa kwa umakini.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Nampongeza
 (Rais Kikwete) kwa kuteua watu wengine. Ni watu wazuri na nawafahamu; 
Dk Mwakyembe amebobea katika sheria na Tizeba ni mhandisi mwenzangu,” 
alisema.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Aliongeza: &quot;Naamini hawa wataweza kusukuma gurudumu la Wizara ya Uchukuzi na kutekeleza kikamilifu Ilani ya CCM.”&lt;br&gt;&lt;br&gt;Ingawa
 kwa sasa hana mamlaka kwenye wizara hiyo, lakini alisema yuko tayari 
kutoa mchango wake pale ambapo watamhitaji kwa ushauri.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kuhusu 
mkakati wake kwa sasa, Mfutakamba alisema ataingia bungeni akiwa mbunge 
wa kawaida na atashirikiana na wenzake katika kuishauri Serikali katika 
mambo mbalimbali ili kuwaletea maendeleo Watanzania.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Nundu&lt;br&gt;&lt;br&gt;Aliyekuwa
 Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu alisema asingependelea kuzungumza na 
vyombo vya habari kwa sasa kwa sababu yeye sasa siyo waziri bali ni mtu 
wa kawaida.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Samahani sana. Sizungumzi na magazeti. Mimi siyo waziri tena ni mtu &apos;private&apos; (mtu binafsi),&quot; alisema Nundu na kukata simu. &lt;br&gt;&lt;br&gt;Mkulo&lt;br&gt;&lt;br&gt;Aliyekuwa
 Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo naye alisisitiza kuwa hayuko 
tayari kuzungumza kupitia vyombo vya habari kwa sasa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Hakupenda kutoa sababu za kuwa na msimamo huo baada ya kukata simu iliasiendelee kuhojiwa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Miongoni
 mwa mawaziri wengine ambao waliachwa kwenye baraza hilo ni waliokuwa 
Mawaziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, Afya na Usatawi wa Jamii, 
Dk Haji Mpona, Naibu wake, Dk Lucy Nkya, Nishati na Madini, Wiliam 
Ngeleja na Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Dk Mponda na Dk Nkya simu zao zilikuwa zimefungwa wakati wengine zilikuwa zinaita kwa muda mrefu bili kupokelewa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wabunge wateule watoa neno&lt;br&gt;&lt;br&gt;&lt;br&gt;Nao
 wabunge wateule wamesema ili kuepusha mvutano baina ya Serikali na 
jamii viongozi nchini wanatakiwa kuwajibika na kuwa karibu zaidi na 
wananchi huku mmoja wao, Profesa&amp;nbsp; Sospeter Muhongo akisita kuzungumza 
kuteuliwa kwake kwa sasa na kufafanua kuwa wanasayansi sio wanasiasa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wabunge
 hao walioteuliwa juzi na Rais Jakaya Kikwete ni Mwenyekiti wa Chama cha
 NCCR-Mageuzi, James Mbatia, Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, 
Sospeter Muhongo, kada wa CCM, Janet Mbene na Saada Mkuya.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wakizungumza
 na Mwananchi kwa nyakati tofauti, Mbene ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati 
ya Uchumi ya chama hicho jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Serikali 
ya Mtaa wa Masaki alisema yupo tayari kuwatumikia wananchi&amp;nbsp; kwa kuwa ni 
mzalendo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mbene ambaye aliwahi kuteuliwa na Rais kuwa Mbunge 
Februari 2010 alisema viongozi wanatakiwa kuwa karibu na wananchi ikiwa 
ni pamoja na kuwashirikisha na kuwasikiliza matatizo yao.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Tusipofanya
 hivyo wananchi wanaweza kuhisi jambo lolote, inawezekana haya 
yaliyotokea kwa mawaziri yametokana na mambo kutowekwa wazi na kutolewa 
ufafanuzi, wananchi wanatakiwa kupewa ufafanuzi wa masuala mbalimbali, 
pia wapewe huduma muhimu malalamiko yatapungua,”alisema Mbene.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kada
 huyo wa CCM ambaye ameteuliwa na Rais Kikwete kuwa Naibu Waziri wa 
Fedha na Uchumi alisema alisema , &quot;&quot;Ukiwa waziri kazi hufanyi peke yako 
unakuwa na wasaidizi, pia wapo wenzako ambao utawakuta na wana, 
unapopata fursa kama hizi unatakiwa kutumia ulichonacho kwa ajili ya 
wengine”.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mbene aliwahi kugombea ubunge wa Viti Maalum kupitia 
NGO mwaka 2010 lakini alishindwa na Rita Mlaki. Hivi karibuni aliteuliwa
 na Kamati Kuu (CC) ya CCM kuwania Ubunge wa Afrika Mashariki lakini 
alishindwa baada ya kupata kura chache katika uchaguzi uliofanyika 
Bungeni, Dodoma.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Kwa upande wake Mbatia alisema kuwa ameteuliwa 
na Rais kuwa mbunge kutokana na chama chake kuwa na siasa za kujenga 
hoja, siasa&amp;nbsp; ambazo zinawafanya watanzania kudai haki zao bila vurugu na
 kumwaga damu.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alisema kuwa hajachaguliwa kwa upendeleo wala 
kulipa fadhila na kwamba Rais Kikwete amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa 
Katiba ya Jamhuri ya Muungano.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Katiba iko wazi na imeeleza kuwa 
Rais anaweza kuteua mtu yoyote bila kujali anatokea chama gani cha 
siasa. Katika suala zima la uongozi hakuna mwenye hati miliki ya 
kuwaongoza watanzania” alisema Mbatia&lt;br&gt;&lt;br&gt;Mbatia ambaye Januari 21 
mwaka huu akiwa na viongozi wengine wa chama hicho waliitwa Ikulu kutoa 
maoni yao kuhusu Katiba mpya alisema tatizo kubwa linaloikabili nchi ni 
mfumo wa elimu ambao unasababisha mmonyoko wa maadili, ukosefu wa 
uadilifu na uaminifu, wajibikaji wa pamoja na watu kutopenda kufanya 
kazi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&quot;Mfumo huu unawafanya watu kutoiheshimu Katiba na sheria za
 nchi jambo ambalo linasababisha kuwepo na pengo kubwa kati ya mwenye 
nacho na asiyenacho” alisema Mbatia.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Alisema kwakuwa sio mbunge wa kuchaguliwa, jukumu lake kubwa ni kuwatumikia watanzania wote, chama chake.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wakati
 Mbatia akieleza hayo&amp;nbsp; Profesa, Sospeter Muhongo ambaye siku nne 
zilizopita aliteuliwa kuwa mbunge, juzi ameteuliwa tena kuwa Waziri wa 
Nishati na Madini juzi, alisita kuzungumzia uteuzi huo na kusema kuwa 
wanasayansi sio wazungumzaji kwa kuwa sio wanasiasa.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Profesa huyo
 wa Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,&amp;nbsp; Profesa wa heshima ya
 Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Pretoria, Afrika Kusini aliomba atafutwe
 siku nyingine na kuahidi kuwa atazungumza kwa kirefu kuhusu kuteuliwa 
kwake.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Huku akizungumza kwa furaha alisema, &quot;Nisamehe kijana 
wangu unajua wanasayansi si wazungumzaji sana kwa kuwa sio wanasiasa, 
nipe muda kidogo nakuahidi kuwa tutazungumza mengi tu ila kwa sasa nipe muda</content:encoded>
			<link>https://siasa.ucoz.com/news/mawaziri_waanza_kwa_mkwara/2012-05-11-20</link>
			<dc:creator>twangaraha</dc:creator>
			<guid>https://siasa.ucoz.com/news/mawaziri_waanza_kwa_mkwara/2012-05-11-20</guid>
			<pubDate>Fri, 11 May 2012 06:42:53 GMT</pubDate>
		</item>
	</channel>
</rss>