PAMOJA TUNAWEZA KULINDA TANZANIA
Statistics |
Total online: 1 Guests: 1 Users: 0 |
JIUNGE NA CHADEMA UOKOE RASILIMALI ZA TAIFA
KAMA RASILIMALI HAZITAANZA KUWANUFAISHA WANANCHI WA ENEO HUSIKA KATIKA TAIFA KUNA HAATARI YA TAIFA KUINGIA KWENYE VURUGU KAMA ILIVYO KUWA KWA SUDANI KUSINI
|
Main » 2012 » May » 13 » mambo yaenda vibaya,ikulu yapingwa
11:31 AM mambo yaenda vibaya,ikulu yapingwa |
WANAHARAKATI nchini wamepinga mpango wa Ikulu wa kutaka kuwapo na
uchunguzi wa watendaji katika wizara na taasisi nyingine za umma
wanaotuhumiwa kuhusika na ubadhirifu wa fedha za umma kwa kigezo kwamba
ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inatosha
kuwafikisha mahakamani.
Kauli hiyo imekuja baada ya juzi Ikulu
kuagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na
Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) kuwachunguza watendaji hao na kwamba
uchunguzi huo kwa kile walichoeleza ni ili kutomuonea mtu wala
kukandamiza wakati wa kuchukua hatua.
Wakichangia maoni katika
mada ya hali ya uwajibikaji nchini iliyotolewa kwenye Semina ya
Maendeleo na Jinsia (GDSS), iliyofanyika katika viwanja vya Mtandao wa
Jinsia Tanzania (TGNP) jijini Dar es Salaam walisema , tuhuma
zilizowaondoa kwenye nafasi zao ni za kushindwa kuwajibika na si za
rushwa.
Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Jinsia katika mtandao huo,
Diana Mwiru alisema kwa sasa hakuna haja ya kufanya uchunguzi kwa kuwa
ripoti ya CAG na zile za kamati tatu za Bunge zinaonyesha wazi namna
wahusika walivyohusika katika tuhuma hizo.
"Tuhuma zinazowahusu
mawaziri zinatokana na wao kushindwa kuwajibika na kulisababishia hasara
taifa, … ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za serikali (CAG) na ripoti za
kamati tatu za Bunge zote ziko wazi na wote tumeona hasara iliyotokea
,hoja yangu ni kwamba tunachunguza nini tena? alihoji Mwiru na kuongeza:
"Kinachotakiwa
kwa sasa ni wahusika kufikisha mahakamani kujibu tuhuma, unafanyika
uchunguzi mwingine wa nini, hawa wanatufanya sisi hatujui kitu, kazi ya
Takukuru ni kuchunguza rushwa swali ni je tuhuma hizo ni za rushwa?
alihoji Mwiru.
Mwiru alisisitiza kuwa chunguzi zilizofanywa
zinatosha na sasa Watanzania wanataka kuona watuhumiwa wakifikishwa
kwenye mhimili mwingine unaotafsiri sheria (Mahakama) ili kuona haki
inatendeka.
Mawaziri waliondolewa katika nafasi zao walitajwa
katika ripoti ya CAG, na pia ripoti za kamati za kudumu za Bunge
zilizowasilishwa kwenye vikao vya Bunge lilifanyika hivi karibuni mkoani
Dodoma.
Kamati hizo ni ile ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za
Serikali na Mashirika ya Umma (POAC) ambayo Mwenyekiti wake ni Mbunge wa
Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na
Mazingira Mwenyekiti wake , James Lembeli zilionyesha namna mawaziri
walivyoshindwa kuwajibika na kusababishia taifa hasara kubwa.
Ripoti
za kamati hizo bungeni ziliibua tuhuma za upotevu wa fedha huku
zikiwataja baadhi ya mawaziri kushindwa kuwajibika hali iliyomsukuma
Mbunge wa Kigoma kaskazini, Zitto Kabwe kuitisha hoja ya kukusanya saini
za kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Akitoa
mada katika washa hiyo, Amina Uddy mwanaharakati kutoka ForDIA, alisema
hali ya uwajibikaji nchini imeshuka kwa kiwango kikubwa hali
inayowafanya viongozi washindwe kujali na kusimamia rasilimali za umma.
|
Views: 1409 |
Added by: twangaraha
| Rating: 0.0/0 |
|
|
|