PEEEEEOPLE'S POOOOOOOWEEEEEER NGUVU YA UMMAAA
Friday, 2024-04-19
My site
PAMOJA TUNAWEZA KULINDA TANZANIA
Site menu
Our poll
Rate my site
Total of answers: 3
Statistics

Total online: 1
Guests: 1
Users: 0
JIUNGE NA CHADEMA UOKOE RASILIMALI ZA TAIFA KAMA RASILIMALI HAZITAANZA KUWANUFAISHA WANANCHI WA ENEO HUSIKA KATIKA TAIFA KUNA HAATARI YA TAIFA KUINGIA KWENYE VURUGU KAMA ILIVYO KUWA KWA SUDANI KUSINI
Main » 2012 » May » 22
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemaliza uchaguzi katika ngazi ya mashina na matawi huku kikikabiliwa na tatizo la kupata wagombea nafasi ya mabalozi wa nyumba kumi katika maeneo mbalimbali nchini.Uchunguzi wa gazeti hili katika mikoa mbalimbali, umebaini kuwa makada wengi wa CCM walikwepa kugombea nafasi hiyo jambo lililofanya walazimishane na kuleta wakati mgumu kupata warithi.

Kwa mujibu wa Katiba ya CCM, mabalozi au wajumbe wa shina ndio ngazi ya kwanza ya uongozi ndani ya chama hicho pia ni kiungo muhimu kati ya chama na wananchi katika maeneo wanayoishi.

Mbali ya majukumu mengine, mabalozi wa nyumba kumi wamekuwa wahamasishaji wakuu wa chama katika maeneo yao, kuhakikisha wanachama wanajiandikisha kwenda kupiga kura pia kujua idadi yao kwenye eneo husika.

Katibu wa CCM Wilaya ya Dodoma Mjini, Augustino Mbogo, amekiri kuwa kazi ya kuchagua mabalozi wa nyumba kumi iliingia dosari na kufanya baadhi ya watu kususa.

Hata hivyo, aliwarushia lawama ... Read more »
Views: 14255 | Added by: twangaraha | Date: 2012-05-22 | Comments (2)

SAKATA la Mbunge wa Maswa Mashariki, John Shibuda kutangaza nia ya kuwania urais ndani ya Kikao cha Halmashauri Kuu (Nec) ya CCM, sasa linaitikisa Chadema baada ya Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la chama hicho (Bavicha), Joliana Shonza kupingana hadharani na bosi wake, John Heche.

Wakati Heche akiwa tayari ametoa tamko kumshambulia Shibuda akisema chama hicho hakitaruhusu mgombea wake urais  atangaze nia kwenye vikao vya CCM, Shonza ameibuka na kusema tamko hilo la bosi wake siyo la Bavicha ila ni lake binafsi.

Jana, Shonza akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, alilikana tamko la Heche wiki iliyoipita akisema hakuna kikao ambacho baraza hilo lilikaa na kutoa kauli moja kumjadili Shibuda.

Hii ni mara ya tatu kwa Shibuda kusababisha mgongano ndani ya Chadema. Aliwahi kupinga msimamo wa kutotambua matokeo ya urais wa Jakaya Kikwete na badala yake, alishiriki tafrija Ikulu ndogo Chamwino, baada ya mkuu huyo wa nchi kuzindua Bunge la 10 n ... Read more »

Views: 3930 | Added by: twangaraha | Date: 2012-05-22 | Comments (0)

KASHFA nyingine imeibuliwa katika Idara ya Uhamiaji.Taarifa mpya yenye kurasa tano, imewataja vigogo hao saba wakidaiwa kuwa na utajiri wa kutisha.Taarifa hiyo ambayo tunayo nakala yake, imedai kuwa vigogo hao wanamiliki mali na mamilioni ya shilingi katika akaunti zao binafsi.

Maofisa saba wametajwa kwa majina na vituo vyao vya kazi ambavyo ni Lindi, Dar es Salaam, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) na Moshi.

Tuhuma hizo zimekuja wakati Tume Maalumu iliyoundwa kuchunguza tuhuma za ufisadi na utoaji wa vibali bandia kwa wageni, ikitajwa kuanza kazi juzi. Hata hivyo, habari kutoka wizarani zinaeleza kuwa timu hiyo itaanza rasmi kazi zake leo.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Uhamiaji, zimedai kuwa baadhi ya wajumbe wa tume hiyo wamemhoji meneja wa benki moja kubwa ya Moshi ili kupata ukweli wa madai kuwa kigogo mmoja wa Uhamiaji mwenye cheo cha Naibu Kamishna (DCI), anamiliki akaunti ya fedha za kigeni.

Kigogo huyo anahusishwa pia na mtan ... Read more »

Views: 8039 | Added by: twangaraha | Date: 2012-05-22 | Comments (1)

Login form
Calendar
«  May 2012  »
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031
NATHASON THE GREAT © 2024