PEEEEEOPLE'S POOOOOOOWEEEEEER NGUVU YA UMMAAA
Friday, 2024-03-29
My site
PAMOJA TUNAWEZA KULINDA TANZANIA
Site menu
Our poll
Rate my site
Total of answers: 3
Statistics

Total online: 1
Guests: 1
Users: 0
JIUNGE NA CHADEMA UOKOE RASILIMALI ZA TAIFA KAMA RASILIMALI HAZITAANZA KUWANUFAISHA WANANCHI WA ENEO HUSIKA KATIKA TAIFA KUNA HAATARI YA TAIFA KUINGIA KWENYE VURUGU KAMA ILIVYO KUWA KWA SUDANI KUSINI
Main » 2012 » May » 11 » Mawaziri waanza kwa mkwara
10:42 AM
Mawaziri waanza kwa mkwara
SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kufanya mabadiliko makubwa katika Baraza lake la mawaziri, mawaziri na manaibu wapya wamesema watahakikisha wanafanya kazi kwa maslahi ya Taifa na Watanzania.

Juzi Rais Kikwete alifanya uteuzi huo kwa kufanya mabadiliko makubwa ya Baraza lake kwa kuingiza sura 13 mpya huku mawaziri na naibu mawaziri nane wakitupwa nje ya baraza hilo.

Katika mabadiliko hayo, amewapandisha naibu mawaziri wanne kuwa mawaziri kamili na kuwahamisha mawaziri nane na naibu mawaziri sita, huku mawaziri na naibu mawaziri 22 wakibaki katika wizara zao za awali.

Dk Mgimwa

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi Jumapili Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk William Mgimwa, alisema uteuzi huo ni jambo la heshima hivyo ni lazima kujituma na kufanya kazi kwa maslahi ya Watanzania.

Alipoulizwa jinsi atakavyokabiliana na changamoto ndani ya wizara hiyo ikiwa ni pamoja na tuhuma zilizomng ‘oa aliyekuwa waziri wa wizara hiyo Mustapha Mkulo, Dk Mgimwa ambaye ni Mbunge wa Kalenga alisema kabla ya kufanya lolote ni lazima kujiridhisha.

"Bungeni tulikuwa tunazungumza mengi kuhusu wizara hii lakini niseme kwamba ni lazima ufanye tathmini na ukishajua hali halisi ya tatizo ndio unaweza kuzungumza suluhisho la tatizo husika ni nini, hakuna kisichowezekana,” alisema Dk Mgimwa

Alisema atafanya kazi kwa kujituma na uzalendo mkubwa ili kuhakikisha makusanyo ya fedha yanaongezeka, matumizi ya fedha yanafanyika kama yalivyopangwa na  kuboresha ukusanyaji wa mapato.

Makamba

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano, January Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli, alisema moja ya mambo ya kufanya katika wizara hiyo ni kuitazama upya gharama za mitandao ya simu, mitandao kutofika maeneo ya vijijini pamoja na huduma hiyo kuwa bora zaidi.

"Wizara hii inagusa maisha ya kila siku ya Mtanzania hivyo kuna ulazima wa kutizama gharama za mitandao ya simu ili iendane na maisha halisi ya mtanzania” alisema Makamba.

Akizungumzia masuala ya sayansi, Makamba alisema kuwa kuna ulazima wa kutizama upya msingi wa elimu ya sayansi kuanzia shule ya msingi kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi, lengo likiwa ni kuongeza idadi ya wanafunzi wanaosoma somo hilo.

Pia, aligusia mikakati iliyowekwa awali ya asilimia moja ya pato la taifa kuingizwa katika ufanyaji wa tafiti mbalimbali na kwamba umefikia wakati wa suala hilo kuanza kutekelezwa kikamilifu.

"Tunatakiwa kuondoa urasimu wa matumizi ya teknolojia, hakuna haja ya watumishi wa Serikali na wananchi kupanga foleni kwa ajili ya kuchukua fomu, huu ni wakati wa fomu kujazwa katika mitandao tu,” alisema Makamba.

Hata hivyo, Makamba alisema kuwa mambo mengi anayoyaona na kuyazungumza hata bungeni yameshaanza kufanyiwa kazi na wizara hiyo.

Rashid

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Suleiman Rashid alisema kuwa kipaumbele katika wizara hiyo ni kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi, tena kwa ubora mkubwa.

"Huduma ya afya inatakiwa kuwafikia watu wote nchini ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mgonjwa anasafirishwa eneo moja mpaka jingine kwa usalama” alisema Dk Rashid.

Rashid ambaye pia ni Mbunge wa Rufiji alisema kuwa wizara inatakiwa kushughulikia sera na kutengeneza mipango mizuri ili watumishi wake wafanye kazi katika mazingira bora kwa faida yao na Watanzania wote.

Tizeba

Naye Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba ambaye ni Mbunge wa Buchosa alisema kwa kuwa ni msaidizi wa waziri wa wizara hiyo, Dk Harrison Mwakyembe, atahakikisha kila jambo analofanya bosi wake linakwenda sawa.

"Namshuruku sana Rais Kikwete, Waziri Mkuu na Makamu wa Rais kwa kuwa wao ndio waliopendekeza mimi kuteuliwa kuwa waziri, nitatumia elimu  yangu na uzoefu katika Serikali katika utendaji wangu wa kazi” alisema Dk Tizeba.

Mahenge

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Wizara ya Maji, Dk Binilith Mahenge ambaye ni Mbunge wa Makete, alisema kuwa atazungumza zaidi mara baada ya kuapishwa.

Masele
Akizungumzia kuteuliwa kwake Masele alisema kwanza atapambana kudhibiti mali ya umma, kuhakikisha udhibiti wa madini na kupata thamani halisi ya kile kinachozalishwa.

Pia alisema atashughulikia matatizo ya wachimbaji wadogo ambao wamekuwa wakinyonywa ili waweze kupata haki zao stahiki na kuinua uchumi wao.

"Niwahakikishie Watanzania kwamba nimepewa nafasi kubwa na nitafanya kazi kwa uadilifu,"alisema Masele.

Aliongeza kuwa; "Tutahakikisha tunazipitia sheria na kuhakikisha wamiliki wa migodi wanawasaidia wananchi na kila sehemu ulipo mgodi tutashughulikia ili wananchi na serikali vyote vinufaike."

Alisema kuna watu wanapotosha kuhusu elimu yake, lakini ana Shahada ya Sayansi ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa aliyoipata kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) ambako alihitimu mwaka 2004.

Pia amewahi kufanya kazi katika benki kabla ya kupata nafasi ya kuwa Meneja Kanda ya Ziwa wa Kampuni ya Simu ya Mkononi ya Tigo.

Mawaziri walioachwa wazungumza

Baadhi ya Mawaziri waliochwa kwenye baraza la jipya, wameelezea kilicho moyoni mwao katika kipindi hiki ambacho sasa watahudhuria Bunge kama wabunge wa kawaida na watapata fursa ya kuibana Serikali kiutendaji.

Mtufatakamba

Aklizungumza na Mwananchi Jumapili, aliyekuwa Naibu Waziri wa Uchukuzi, Athuman Mfutakamba alisema: "Kwanza namshukuru Mheshimiwa Rais (Jakaya Kikwete) kwa kuniteua kuwa Naibu Waziri, kwa kipindi chote cha miaka miwili nimejifunza na nimekumbana na changamoto nyingi.”

Kuhusu baraza lililosukwa upya, Mfutakamba alisema anampongeza Rais Kikwete kwa kuteua watu makini na wenye elimu kusimamia Wizara ya Uchukuzi.

Alisema uteuzi wa Dk Harison Mwakyembe kuwa Waziri wa Uchukuzi na Charles Tizeba kuwa naibu wake, umefanywa kwa umakini.

"Nampongeza (Rais Kikwete) kwa kuteua watu wengine. Ni watu wazuri na nawafahamu; Dk Mwakyembe amebobea katika sheria na Tizeba ni mhandisi mwenzangu,” alisema.

Aliongeza: "Naamini hawa wataweza kusukuma gurudumu la Wizara ya Uchukuzi na kutekeleza kikamilifu Ilani ya CCM.”

Ingawa kwa sasa hana mamlaka kwenye wizara hiyo, lakini alisema yuko tayari kutoa mchango wake pale ambapo watamhitaji kwa ushauri.

Kuhusu mkakati wake kwa sasa, Mfutakamba alisema ataingia bungeni akiwa mbunge wa kawaida na atashirikiana na wenzake katika kuishauri Serikali katika mambo mbalimbali ili kuwaletea maendeleo Watanzania.

Nundu

Aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu alisema asingependelea kuzungumza na vyombo vya habari kwa sasa kwa sababu yeye sasa siyo waziri bali ni mtu wa kawaida.

"Samahani sana. Sizungumzi na magazeti. Mimi siyo waziri tena ni mtu 'private' (mtu binafsi)," alisema Nundu na kukata simu.

Mkulo

Aliyekuwa Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo naye alisisitiza kuwa hayuko tayari kuzungumza kupitia vyombo vya habari kwa sasa.

Hakupenda kutoa sababu za kuwa na msimamo huo baada ya kukata simu iliasiendelee kuhojiwa.

Miongoni mwa mawaziri wengine ambao waliachwa kwenye baraza hilo ni waliokuwa Mawaziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, Afya na Usatawi wa Jamii, Dk Haji Mpona, Naibu wake, Dk Lucy Nkya, Nishati na Madini, Wiliam Ngeleja na Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige.

Dk Mponda na Dk Nkya simu zao zilikuwa zimefungwa wakati wengine zilikuwa zinaita kwa muda mrefu bili kupokelewa.

Wabunge wateule watoa neno


Nao wabunge wateule wamesema ili kuepusha mvutano baina ya Serikali na jamii viongozi nchini wanatakiwa kuwajibika na kuwa karibu zaidi na wananchi huku mmoja wao, Profesa  Sospeter Muhongo akisita kuzungumza kuteuliwa kwake kwa sasa na kufafanua kuwa wanasayansi sio wanasiasa.

Wabunge hao walioteuliwa juzi na Rais Jakaya Kikwete ni Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Sospeter Muhongo, kada wa CCM, Janet Mbene na Saada Mkuya.

Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti, Mbene ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi ya chama hicho jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Masaki alisema yupo tayari kuwatumikia wananchi  kwa kuwa ni mzalendo.

Mbene ambaye aliwahi kuteuliwa na Rais kuwa Mbunge Februari 2010 alisema viongozi wanatakiwa kuwa karibu na wananchi ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha na kuwasikiliza matatizo yao.


"Tusipofanya hivyo wananchi wanaweza kuhisi jambo lolote, inawezekana haya yaliyotokea kwa mawaziri yametokana na mambo kutowekwa wazi na kutolewa ufafanuzi, wananchi wanatakiwa kupewa ufafanuzi wa masuala mbalimbali, pia wapewe huduma muhimu malalamiko yatapungua,”alisema Mbene.

Kada huyo wa CCM ambaye ameteuliwa na Rais Kikwete kuwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi alisema alisema , ""Ukiwa waziri kazi hufanyi peke yako unakuwa na wasaidizi, pia wapo wenzako ambao utawakuta na wana, unapopata fursa kama hizi unatakiwa kutumia ulichonacho kwa ajili ya wengine”.

Mbene aliwahi kugombea ubunge wa Viti Maalum kupitia NGO mwaka 2010 lakini alishindwa na Rita Mlaki. Hivi karibuni aliteuliwa na Kamati Kuu (CC) ya CCM kuwania Ubunge wa Afrika Mashariki lakini alishindwa baada ya kupata kura chache katika uchaguzi uliofanyika Bungeni, Dodoma.

Kwa upande wake Mbatia alisema kuwa ameteuliwa na Rais kuwa mbunge kutokana na chama chake kuwa na siasa za kujenga hoja, siasa  ambazo zinawafanya watanzania kudai haki zao bila vurugu na kumwaga damu.

Alisema kuwa hajachaguliwa kwa upendeleo wala kulipa fadhila na kwamba Rais Kikwete amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

"Katiba iko wazi na imeeleza kuwa Rais anaweza kuteua mtu yoyote bila kujali anatokea chama gani cha siasa. Katika suala zima la uongozi hakuna mwenye hati miliki ya kuwaongoza watanzania” alisema Mbatia

Mbatia ambaye Januari 21 mwaka huu akiwa na viongozi wengine wa chama hicho waliitwa Ikulu kutoa maoni yao kuhusu Katiba mpya alisema tatizo kubwa linaloikabili nchi ni mfumo wa elimu ambao unasababisha mmonyoko wa maadili, ukosefu wa uadilifu na uaminifu, wajibikaji wa pamoja na watu kutopenda kufanya kazi.

"Mfumo huu unawafanya watu kutoiheshimu Katiba na sheria za nchi jambo ambalo linasababisha kuwepo na pengo kubwa kati ya mwenye nacho na asiyenacho” alisema Mbatia.

Alisema kwakuwa sio mbunge wa kuchaguliwa, jukumu lake kubwa ni kuwatumikia watanzania wote, chama chake.

Wakati Mbatia akieleza hayo  Profesa, Sospeter Muhongo ambaye siku nne zilizopita aliteuliwa kuwa mbunge, juzi ameteuliwa tena kuwa Waziri wa Nishati na Madini juzi, alisita kuzungumzia uteuzi huo na kusema kuwa wanasayansi sio wazungumzaji kwa kuwa sio wanasiasa.

Profesa huyo wa Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,  Profesa wa heshima ya Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Pretoria, Afrika Kusini aliomba atafutwe siku nyingine na kuahidi kuwa atazungumza kwa kirefu kuhusu kuteuliwa kwake.

Huku akizungumza kwa furaha alisema, "Nisamehe kijana wangu unajua wanasayansi si wazungumzaji sana kwa kuwa sio wanasiasa, nipe muda kidogo nakuahidi kuwa tutazungumza mengi tu ila kwa sasa nipe muda
Views: 1252 | Added by: twangaraha | Rating: 0.0/0
Total comments: 1
1 StitchSOt  
0
http://funstitch.ru

Name *:
Email *:
Code *:
Login form
Calendar
«  May 2012  »
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031
NATHASON THE GREAT © 2024