JIUNGE NA CHADEMA UOKOE RASILIMALI ZA TAIFA
KAMA RASILIMALI HAZITAANZA KUWANUFAISHA WANANCHI WA ENEO HUSIKA KATIKA TAIFA KUNA HAATARI YA TAIFA KUINGIA KWENYE VURUGU KAMA ILIVYO KUWA KWA SUDANI KUSINI
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemaliza uchaguzi katika ngazi ya mashina na
matawi huku kikikabiliwa na tatizo la kupata wagombea nafasi ya
mabalozi wa nyumba kumi katika maeneo mbalimbali nchini.Uchunguzi wa
gazeti hili katika mikoa mbalimbali, umebaini kuwa makada wengi wa CCM
walikwepa kugombea nafasi hiyo jambo lililofanya walazimishane na kuleta
wakati mgumu kupata warithi.
Kwa mujibu wa Katiba ya CCM,
mabalozi au wajumbe wa shina ndio ngazi ya kwanza ya uongozi ndani ya
chama hicho pia ni kiungo muhimu kati ya chama na wananchi katika maeneo
wanayoishi.
Mbali ya majukumu mengine, mabalozi wa nyumba kumi
wamekuwa wahamasishaji wakuu wa chama katika maeneo yao, kuhakikisha
wanachama wanajiandikisha kwenda kupiga kura pia kujua idadi yao kwenye
eneo husika.
Katibu wa CCM Wilaya ya Dodoma Mjini, Augustino
Mbogo, amekiri kuwa kazi ya kuchagua mabalozi wa nyumba kumi iliingia
dosari na kufanya baadhi ya watu kususa.
Hata hivyo, aliwarushia
lawama baadhi ya watendaji ndani ya chama hicho kwa ngazi ya Kata na
Matawi kuwa walikuwa kikwazo cha kukwamisha mchakato huo na kuwafanya
baadhi ya wanachama kususa. Mbogo alitoa kauli hiyo jana alipokuwa
akielezea namna mchakato wa uchaguzi ndani ya chama unavyoendelea,
ikiwemo uchaguzi wa ngazi ya mashina ambao umefikia kilele hivi
karibuni. Alisema kuwa katika wilaya yake, yako maeneo ambayo
viongozi walitoa taarifa kuwa mabalozi walikuwa wakikataa kugombea na
maeneo mengine waliamua kupeana nafasi hizo bila kufuata taratibu
zozote. "Ni kweli kuna baadhi ya maeneo hali haikuwa nzuri, mfano
Kata za Chihanga,Hombolo na Mtumba tumepata wakati mgumu watu waligoma
kugombea nafasi hizo,’’alisema Mbogo. Kiongozi huyo alibainisha
sababu za wanachama kugomea kugombea nafasi hizo ambapo alisema ni
kutokana na ukiritimba mkubwa uliokuwa ukifanywa na baadhi ya makatibu
wa maeneo husika. "Unajua wale viongozi wa ngazi ya chini ni watu wa
kuchaguliwa, hivyo katika maeneo mengi walikuwa wakipanga safu zao ili
kujijenga na kuwa na mtaji wa wapiga kura pindi watakapoanza kugombea na
wao,’’alisema. Alitolea mfano kuwa baadhi ya maeneo fomu za kugombea
nafasi hizo za mashina zilikuwa zikiuzwa kati ya Sh 5000 hadi 10,000
kinyume na utaratibu jambo lililofanya baadhi ya watu kushindwa
kuzinunua. Wakati Katibu huyo akieleza mchakato huo, uchunguzi
uliofanywa katika baadhi ya maeneo umebainisha kuwa kwa baadhi ya
sehemu, nafasi hizo hazikutangazwa kabisa,hivyo kufanya mabalozi
waliokuwa madarakani waendelee kuongoza hata kama muda umepita. Kata
za Nzuguni, Iyumbu, Makutupora pamoja na maeneo ya Mpunguzi, Zuzu na
maeneo kadhaa ya mjini Dodoma, uchaguzi huo haukufanyika na wengi
hawajui kama mwaka huu ulikuwa ni mwaka wa uchaguzi kwa mabalozi. Kamati ya siasa Arusha yakutana
Uchaguzi
wa Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) wa mashina, matawi na mabalozi
katika wilaya tano za mkoa wa Arusha, umeelezwa kudorora kwa kiasi
kikubwa mwaka huu, huku wilaya za Arusha mjini na Arumeru zikishindwa
kabisa kufanya uchaguzi wa matawi.
Habari za uhakika kutoka ndani
ya chama hicho, ambazo zimethibitishwa na Katibu wa Uenezi na Itikadi
wa CCM Mkoa wa Arusha, Loota Sanare, zimebainisha kuwa, kudorora kwa
chaguzi hizo kumesababisha na sababu mbali mbali ikiwepo hali ya kisiasa
mkoani Arusha.
Sababu nyingine zilizotajwa na baadhi ya
viongozi wa CCM wa wilaya mkoani hapa, ni pamoja na kukosekana
wagombea, na hivyo viongozi waliopo kuendelea kushikilia nafasi zao na
kushindwa kusimamiwa zoezi la uchukuaji fomu, kurejeshwa na kupitisha
majina kutokana na viongozi wengi kushiriki katika uchaguzi mdogo wa
jimbo la Arumeru.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, uchaguzi wa matawi
katika wilaya hasa za Arusha na Arumeru hadi jana ulikuwa haujafanyika,
wakati uchaguzi wa mashina na mabalozi pia haujafanyika kwani wengi wa
mabalozi, wameendelea na nafasi zao.
"Unajua mwaka huu, hapa
Arusha tulikuwa na uchaguzi wa Arumeru kuanzia Januari hadi Aprili
viongozi wengi walikuwa huko, hivyo ilishindikana uratibu wa
chaguzi,"alisema kiongozi huyo.
Hata hivyo, alisema katika wilaya
nyingine za Longido, Monduli, Karatu na Ngorongoro, uchaguzi wa ngazi
za Mashina na matawi zimefanyika kwa wastani wa asilimia 80 tu.
Kutokana
na hali hiyo, Kamati ya Siasa Mkoa wa Arusha, ilitarajiwa kukutana jana
kupokea taarifa za chaguzi hizo na kujua uhai wa chama katika wilaya
zote.
Sanare alisema katika kikao hicho, kila wilaya itakuwa na
ripoti yake ya chaguzi, hivyo kujulikana taarifa sahihi ni maeneo gani
hazijafanyika na sababu zake, pia hatua ambazo zitachukuliwa.
"Naomba
usubiri mara baada ya kikao cha Kamati ya Siasa tutakuwa na taarifa
kamili ya chaguzi hizo na hali ya kisiasa ya mkoa wetu,"alisema Sanare.
Mkoa
wa Arusha ni miongoni mwa mikoa ambayo hali ya kisiasa imekuwa tete kwa
CCM hasa kutokana na viongozi wake na makada kadhaa kujiengua na
kujiunga na chadema.
Kinondoni
Akizungumza jana Mwenyekiti
wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Aron Mwaikambo alisema chaguzi zilizo
tayari ni za jumuiya pamoja na chama ngazi ya ubalozi na matawi.
Mwaikambo
alisema, ubalozi wa nyumba kumi tangu Februari mwaka huu ila hapakuwa
na upinzani kwa sababu sehemu nyingi ni mtu mmoja tu alijitokeza
kugombea, hivyo kushinda bila upinzani.
"Tulifanya uchaguzi wa
nyumba kumi kuanzia Februari 2 hadi 5 mwaka huu tukamaliza zoezi hilo na
tulipenda kungekuwepo na upinzani ila watu walikua wachache na katika
kila eneo la hizo nyumba kumi aliyechukua fomu ndio mshindi kwasababu
hapakua na upinzani kabisa”alisema Mwaikambo.Alieleza:
Sehemu
nyingi wazee wamechoka hivyo wamewaachia vijana nafasi hiyo lakini
asilimia kubwa ya vijana hawakujitokeza kwani licha ya balozi kuwa
anatekeleza kazi za chama, pia ana jukuma la kupatanisha migogoro
inayotokea katika nyumba hizo hasa familia ambapo kwa vijana inakua
ngumu.
Temeke
Wakati hayo yakiendelea Kinondoni Msemaji wa
CCM Wilaya ya Temeke, Saad Kusilawe amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi
kimepata watu wengi waliojitokeza kuchukua fomu za ubalozi wa nyumba
kumi katika kata zake zote.
Akizungumza jana ofisini kwake,
alisema hali ilikuwa tofauti na alivyofikiria kwani waliojitokeza ni
wengi tofauti na kipindi cha nyuma kulikuwa na wanachama wapatao 5,228
na katika kipindi hiki waliokuja kuchukuwa fomu hizo wamefikia 7,800
hali ambayo inaonyesha kuwa chama hicho bado kipo imara.
Kusilawe
alisema hali ya siasa ina changamoto hasa kipindi hiki ambacho vijana
wengi wamejikita katika suala la siasa na kupelekea mambo kubadilika
kutokana na kujitambua kwao.
"kwakweli vijana wamekuja juu sana
kipindi hiki ila kinachoniogopesha ni kuhusu kuja kwao juu ni kwa
kuchochewa na baadhi ya wanasiasa kufanya fujo na siyo kujenga nchi kama
inavyofikiriwa”alisema kusilawe.
Aliongeza kuwa vijana wengi
hivi sasa wamekaa kiushawishi na mara nyingi uacha mambo yanayowapeleka
shule na kuanza kufanya siasa ambayo mara nyingi inakuwa ni hasara kwao
kutokana na fujo wanazo zianzisha.
Dodoma Katibu wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma Mjini, Augustino Mbogo amekiri kuwa
kazi ya kuchagua mabalozi wa nyumba kumi iliingia dosari na kufanya
baadhi ya watu kususa. Hata hivyo, aliwarushia lawama baadhi ya
watendaji ndani ya chama hicho kwa ngazi ya Kata na Matawi kuwa walikuwa
ni kikwazo cha kukwamisha mchakato huo na kuwafanya baadhi ya watu
kususia.
Mbogo alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akielezea namna
mchakato wa uchaguzi ndani ya chama unavyoendelea ikiwemo uchaguzi wa
ngazi ya mashina ambao umefikia kilele mwishoni mwa wiki.
Alisema
kuwa katika wilaya yake yako maeneo ambayo viongozi walitoa taarifa
kuwa mabalozi walikuwa wakikataa kugombea na maeneo mengine waliamua
kupeana nafasi hizo bila kufuata taratibu zozote.
"Ni kweli kuna
baadhi ya maeneo hali haikuwa nzuri, mfano Kata za Chihanga, Hombolo na
Mtumba tumepata wakati mgumu watu waligoma kugombea nafasi
hizo,’’alisema Mbogo.
Kiongozi huyo alibainisha sababu za
wanachama kugomea kugombea nafasi hizo ambapo, alisema ni kutokana na
ukiritimba mkubwa uliokuwa ukifanywa na baadhi ya makatibu wa maeneo
husika.
"Unajua wale viongozi wa ngazi ya chini ni watu wa
kuchaguliwa, hivyo katika maeneo mengi walikuwa wakipanga safu zao ili
kujijenga na kuwa na mtaji wa wapiga kura pindi watakapoanza kugombea na
wao,’’alisema.
Alitolea mfano kuwa baadhi ya maeneo fomu za
kugombea nafasi hizo za mashina zilikuwa zikiuzwa kati ya Sh 5000 hadi
10,000 kinyume na utaratibu jambo lililofanya baadhi ya watu kushindwa
kuzinunua.
Wakati Katibu huyo akieleza mchakato huo, uchunguzi
uliofanywa katika baadhi ya maeneo umebainisha kuwa katika maeneo mengi
nafasi hizo hazikutangazwa kabisa, hivyo kufanya mabalozi waliokuwa
madarakani waendelee kuongoza hata kama muda umepita.
Hofu ya
kutotangaza inatokana na ukweli kuwa baadhi ya mabalozi hawapendi
kuendelea kuongoza na hivyo kama nafasi hizo zingetangazwa, ni wazi kuwa
wangeweza kuziachia huku chama kikikosa mgombea katika eneo husika. Kata
za Nzuguni, Iyumbu, Makutupora pamoja na maeneo ya Mpunguzi,Zuzu na
maeneo kadhaa ya mjini Dodoma, uchaguzi huo haukufanyika na wengi
hawajui kama mwaka huu ulikuwa ni mwaka wa uchaguzi kwa mabalozi.
Mara Uchaguzi
ngazi ya mashina na matawi ya ya CCM umeshindwa kufanyika katika
maeneo mbalimbali wilayani Serengeti ,kutokana na wanachama wengi kususa
kujitokeza, hali iliyosababisha watu wateuliwe kushika ubalozi kinyume
na utaratibu wa kawaida wa chama wa kupigiwa kura.
Uchunguzi wa
Mwananchi Jumapili ulibaini kuwa nafasi nyingi za ubalozi wa mashina
zimekimbiwa na wanachama wa CCM na sasa waliotayari wanateuliwa kujaza
nafasi hizo.
"Hii ni aibu kubwa na haijawahi kutokea maana ilipofika kipindi hiki cha uchaguzi, watu walifukuzana kuwania ubalozi ,lakini
leo mtu akionekana anachukua fomu ya ubalozi watu wanamzoea, hakika
chama kinakwenda pabaya,”alisema Katibu mmoja wa Tawi la CCM, jina
limehifadhiwa.
Katika Kata ya Manchira, mbali na uteuzi wa
mabalozi na wengine kukataa uteuzi hata uchaguzi wa viongozi ngazi ya
tawi uliokuwa ufanyike mwishoni mwa wiki hii ulishindikana baada ya
wanachama wakiwemo waliochukua fomu, kutojitokeza.
Habari za
uhakika na zilizothibitishwa na baadhi ya viongozi wa matawi na Kata wa
chama hicho, zinadai katika Tawi la Rwamchanga, walijitokeza watu
wasiozidi wanane, hali iliyomlazimisha Katibu wa Uchumi wa Kata hiyo,
John Wambura ambaye alikuwa msimamizi, kuahirisha hadi Mei 21 mwaka huu.
Hali hiyo pia iliyakumba matawi ya Ntamyo,Miserere na Miseke ambapo
wanachama hawakujitokeza hata waliojaza fomu za kuwania nafasi
mbalimbali ,huku kukiwa na uvumi kuwa wana mpango wa kujiungua Chadema
na wanasubiri viongozi wa kitaifa wahame.
Mwenyekiti wa CCM
Wilaya, Patrick Chandi alikiri kuwepo kwa migogoro baadhi ya maeneo
ambapo amelazimika kumwagiza Katibu wake wa wilaya kufuatilia chanzo cha
matatizo.
"Kwa ujumla tunaendelea ingawa kuna mambo hayawezi kwenda sawa sawa. Maeneo kama Rwamchanga,Tamukeri ,Kisaka na kwingineko kuna migogoro ya ndani kwa ndani,”alisema.
503/ст Металлический гимнастический комплекс с неопреновыми ручками и мягкими.Минимальный размер инвестиций, необходимых для того чтобы наладить производство, составляет от 5 миллионов рублей и выше. Однако, если у вас есть возможность сделать вложения в данный производственный процесс, можете не сомневаться: такой бизнес отличается высокой рентабельностью. Довольно скоро даже начинающий предприниматель сможет выйти на безубыточный объем. http://eurocups.ru/seas/34/ http://www.spurs.ru/tottenham-hotspur-video/son-khyn-min-my-rasstroeny-nichejj-s-sheffildom/ https://www.spainland.ru/modules.php?name=Topics
Спасибо, нам спорткомплекс очень понравился.Подтверждение качества - международные сертификаты, на товары всех наших категорий, санитарно-гигиенические заключения МОЗ Украины и сертификаты соответствия нормам ДСТУ. Предоставляем индивидуальную гарантию на весь ассортимент продукции, представленной на сайте, и общую 14-дневную гарантию, согласно Закона о правах потребителя.
http://maxi-driver.pl/wynajmowanie-samochodow Looking for a used or new auto might be a difficult procedure if you do not know what you are doing. By teaching yourself about car shopping before you decide to go to the dealer, you possibly can make issues much easier yourself. The following tips will help your next shopping vacation be a little more pleasant.
Usually deliver a auto mechanic alongside when looking for a whole new automobile. Vehicle dealers are well known for selling lemons and you do not desire to be their following sufferer. When you can not get yourself a auto mechanic to consider cars together with you, no less than make sure that you have him take a look at closing choice before buying it.
Know your boundaries. Before starting shopping for your car or vehicle, decide what you can manage to pay, and follow it. Don't forget to feature desire for your calculations. You will definitely pay out close to 20 % as a down payment also, so be ready.
Prior to going to a car dealership, know what kind of automobile you want. Research each one of you choices ahead of shopping so that you can figure out what works best for your financial allowance and family demands. Seek information to find out exactly how much you must pay for any probable vehicle.
Prior to signing any commitment spend some time to go through each and every range, like the fine print. If you have anything at all detailed you do not understand, usually do not signal before you get an response that you simply understand. Unsavory salesmen can make use of a binding agreement to place numerous fees that have been not talked about.
When you maintain the previous guidance in your mind when which you go looking for a car, you may be more prone to get a better offer. Purchasing a vehicle does not have to become frustration. Simply use the ideas with this write-up and you will obtain the auto you would like at a very good selling price.