PAMOJA TUNAWEZA KULINDA TANZANIA
Statistics |
Total online: 1 Guests: 1 Users: 0 |
JIUNGE NA CHADEMA UOKOE RASILIMALI ZA TAIFA
KAMA RASILIMALI HAZITAANZA KUWANUFAISHA WANANCHI WA ENEO HUSIKA KATIKA TAIFA KUNA HAATARI YA TAIFA KUINGIA KWENYE VURUGU KAMA ILIVYO KUWA KWA SUDANI KUSINI
|
Main » 2012 » May » 17 » poleni sana CCM huu ndio mwisho wenu
2:37 AM poleni sana CCM huu ndio mwisho wenu |
mwalimu nyerere ambaye ndiye mwasisi wa chama cha mapinduzi aliwahi kukitabilia kifo chama ambacho yeye aliki asisi kwa madai kua kina kanza ya uongozi hebu tupate nukuu ya maneno yake kabla htuja endelea
Mwaka 1993 Mwalimu alichapisha kitabu kiitwacho Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (Harare: Zimbabwe Publishing House, 1993). Pamoja na mambo mengine katika kitabu hiki, Mwalimu alisema kuwa kuna kansa katika uongozi wa CCM. Nanukuu baadhi ya maneno yake: ... Chama cha Mapinduzi, kwa sababu ya uzito wa historia yake, hadhi ya jina lake, mfumo wa wavu wake, mazoea ya watu, na ubovu wa Vyama vya Upinzani, kinaweza kuchaguliwa na Watanzania, pamoja na kansa ya uongozi wake. Au watu wanaweza wakachoka, wakasema, "potelea mbali:" wakachagua Chama cho chote, ilimradi tu watokane na kansa ya uongozi wa CCM. Hainifurahishi kuyasema haya, lakini uhai wa Nchi yetu unataka yasemwe. (Ukurasa 61) Mwalimu hakuishia hapo, bali aliongezea namna hii: Nilisema awali kwamba kansa ya uongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona Chama kizuri cha upinzani kinachoweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM. Ubovu wa uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa Vyama Vingi. Nilitumaini kuwa tunaweza kupata Chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM; au ambacho kingekilazimisha Chama cha Mapinduzi kusafisha uongozi wake, kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao. Lakini bado sijakiona Chama makini cha upinzani; na wala dalili zo zote za kuondoa kansa ya uongozi ndani ya CCM. Bila upinzani mzuri wa nje, na bila demokrasia halisi ndani ya Chama cha Mapinduzi, Chama hiki kitazidi kudidimia chini ya uzito wa uongozi mbovu. Kwa hali yetu ya kisiasa ilivyo nchini hili si jambo la kutarajia bila hofu na wasi wasi!(Ukurasa 66)
miaka 19 baada ya mwalimu kusema hayo ameibuka kada mwingine wa chama hicho akiwa na madai sawa na ya mwalimu licha ya yeye mwenyewew kuwa badio sio mtu safi kwenye macho ya watanzania
sasa hali imekuwa mbaya ndani ya ccm badala ya kujadili wafanye nini kukinusuru chama sasa wanajadili na kukosoa vibaya mapungufu makubwa waliyo nayo makada wake licha ya kukili kuwa kasi ya peoples pwa inawabana koo
huo ndio mwisho wenu ndugu zangu wa ccm
|
Views: 1398 |
Added by: twangaraha
| Rating: 0.0/0 |
|
|
|